logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wazazi wa Shule ya Upili ya Kakamega kulipa Sh21.6m kukarabati bweni lililoteketea kwa moto

Kundi la kwanza la wanafunzi linatarajiwa kurudi Jumatatu, Novemba 15.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri11 November 2021 - 14:24

Muhtasari


  • Katika barua kwa wazazi wote ya Novemba 11, Sh21, 611,350 ziliafikiwa baada ya kikao cha bodi mnamo Novemba 10
Moto mkubwa

Wanafunzi wa Shule ya Upili ya Kakamega watalipa jumla ya Sh21.6 milioni kukarabati uharibifu uliotokea mnamo Novemba 6 wa moto ulioteketeza bweni.

Katika barua kwa wazazi wote ya Novemba 11, Sh21, 611,350 ziliafikiwa baada ya kikao cha bodi mnamo Novemba 10.

Kulingana na usimamizi wa shule, uharibifu halisi kulingana na tathmini ya Wizara ya Uchukuzi, Miundombinu na Makazi ni Sh12.1 milioni.

Uongozi pia ulichangia Sh695,420 kwa gharama ya ufungaji wa CCTV katika bweni ambalo bado halijajengwa, na vitanda 280 vya ghorofa mbili vikiwa Sh4.1 milioni na kufikisha Sh21.6 milioni.

Kila mmoja wa wanafunzi 2,200 ameagizwa kulipa Shilingi 9,823 siku ya kuripoti ili kukarabati bweni.

Kundi la kwanza la wanafunzi linatarajiwa kurudi Jumatatu, Novemba 15.

"Jumla ya uharibifu ni Sh21.6 milioni, ikigawanywa na wanafunzi 2,200, kila mwanafunzi atalipa Sh9,832," ilisema barua hiyo.

Wazazi pia wameagizwa kumaliza ada zote ambazo hazijalipwa za Muhula wa Pili.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved