logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Uhuru aomboleza rais wa zamani wa Afrika Kusini FW de Klerk

Klerk alikuwa mkuu wa nchi kati ya Septemba 1989 na Mei 1994.

image
na Radio Jambo

Burudani12 November 2021 - 08:34

Muhtasari


  • Klerk alikuwa mkuu wa nchi kati ya Septemba 1989 na Mei 1994
  • Alikuwa rais wa mwisho mweupe wa Afrika Kusini

Rais Uhuru Kenyatta Ijumaa alifariji Afrika Kusini kufuatia kifo cha aliyekuwa Rais Frederik Willem de Klerk.

Katika ujumbe wake, Uhuru alimkumbuka Klerk kwa kuwa na jukumu muhimu katika kuhakikisha nchi inapita bila ubaguzi wa rangi hadi demokrasia.

Alikuwa rais wa mwisho mweupe wa Afrika Kusini.

"Mheshimiwa Rais Uhuru Kenyatta ametuma ujumbe wa rambirambi na faraja kwa Rais @CyrilRamaphosa na watu wa Jamhuri ya Afrika Kusini kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkuu wa Nchi hiyo Frederik Willem de Klerk," taarifa kutoka Ikulu ilisema.

Klerk alikuwa mkuu wa nchi kati ya Septemba 1989 na Mei 1994.

Kifo chake kilitangazwa Alhamisi, Novemba 11.

“Bw de Klerk, 85, aliwahi kuwa Mkuu wa Serikali ya Afrika Kusini kati ya 1989 na 1994, na alichangia pakubwa katika kipindi cha mpito cha demokrasia kutoka kwa utawala wa kibaguzi nchini humo, jambo ambalo lilimletea Tuzo ya Amani ya Nobel mwaka 1993 pamoja na Rais wa zamani Nelson Mandela. "

Hata hivyo, jukumu lake katika kipindi cha mpito kuelekea demokrasia lilipingwa sana. Mwaka jana, alijiingiza katika mzozo uliofanya ashtumiwe kwa kudharau uzito wa ubaguzi wa rangi. Baadaye aliomba radhi kwa "kubisha" juu ya suala hilo.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved