Covid-19: Watu 3 waaga dunia,Idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika 6,083,449

Muhtasari
  • Vile Vile watu 3 wameaga dunia kutokana na maambukizi ya corona huku idadi jumla ya walioaga dunia ikifika 5,322
  • Kuna wagonjwa 385 ambao wamelazwa hospitalini, 1,021 wamejitenga nyumbani
  • Vile vile kuna wagonjwa 23 katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU)
Image: HISANI

Kenya siku ya mesajili visa 75 vipya vya maambukizi ya Covid-19 kutoka kwa sampuni 3,854 chini ya saa 24 zilizopita.

Kati ya maambukizi hayo 62 ni wakenya huku 13 wakiwa raia wa kigeni,40 ni wanaume huku  35 wakiwa wanawake.

Idadi jumla ya watu waliopatwa na corona nchini imefika 254,384 na kiwango cha maambukizi cha asilimia 2.0%.

Idadi ya sampuli zilizopimwa nchini imefika 2,775,646.

Aidha watu 29 wamepona,Idadi ya waliopona sasa ni 247,711,17 wamepona wakiwa wanapokea matibabu wakiwa nyumbani ilhali 12 wameruhusiwa kuenda nyumbani kutoka hospitali tofauti.

Vile Vile watu 3 wameaga dunia kutokana na maambukizi ya corona huku idadi jumla ya walioaga dunia ikifika 5,322.

Kuna wagonjwa 385 ambao wamelazwa hospitalini, 1,021 wamejitenga nyumbani.

Vile vile kuna wagonjwa 23 katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU).

Idadi ya watu waliopokea chanjo ya corona imefika 6,083,449.