logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Arsenal yashtakiwa na shirikisho la soka FA

KFC ndio kampuni ya hivi punde zaidi kukumbwa na usumbufu wa Covid.

image
na Radio Jambo

Habari05 January 2022 - 12:20

Muhtasari


  • Tukio hilo lilitokea dakika ya 59 baada ya beki wa Gunners, Gabriel kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kupokea kadi ya pili ya njano

Klabu ya Arsenal imeshtakiwa na Shirikisho la soka Uingereza FA kwa kushindwa kuhakikisha wachezaji wao wanajiendesha kwa utaratibu ufaao wakati wa mechi ya Jumamosi dhidi ya Manchester City.

Tukio hilo lilitokea dakika ya 59 baada ya beki wa Gunners, Gabriel kutolewa nje kwa kadi nyekundu baada ya kupokea kadi ya pili ya njano.

Arsenal wana hadi Januari 7 kujibu

KWINGINEKO NI KUWA;

KFC yaahidi kununua viazi vya Kenya baada ya malalamiko

Kampuni ya vyakula ya KFC, imewaahidi wateja wa Kenya kwamba itavinunua viazi vya nchini humo kufuatia lalama kwamba huwa inaagiza viazo kutoka nje.

Migahawa yake nchini Kenya ilikuwa imeacha kutoa vibanzi au chipsi kwa sababu ya changamoto za usafirishaji zilizosababishwa na Covid.

Lakini Wakenya walieleza kuwa wakulima wa eneo hilo walikuwa na akiba ya kutosha ya viazi.

Baadhi kwenye mitandao ya kijamii walitaka KFC isusiwe, wakihoji ni kwa nini ilihitaji kuleta viazi hivyo kutoka Misri.

Mwakilishi wa kampuni hiyo alisema wasambazaji walilazimika kupitia uhakikisho wa ubora.

KFC ndio kampuni ya hivi punde zaidi kukumbwa na usumbufu wa Covid.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved