logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ngilu amtetea Kalonzo, amtaka Ruto akome kuwatusi viongozi

Ngilu alisema tofauti kati ya viongozi hao wawili ni kwamba Kalonzo ni mwaminifu na mtu mwingine sio.

image
na

Yanayojiri22 January 2022 - 09:37

Muhtasari


  • Kupitia kwenye ukuraa wake wa Facebook Jumamosi, Ngilu alisema hawatamruhusu Ruto kuja Ukambani na kumtusi kiongozi wao mwadilifu

DP William Ruto anafaa kuacha kuwatusi viongozi, gavana wa Kitui Charity Ngilu amesema.

Ngilu alikuwa akirejelea matamshi ya Ruto kuwa kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka amepoteza nywele kwa kumuunga mkono kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga.

“Ruto anafaa kuacha kuwatusi viongozi na maeneo ambayo viongozi hao wanatoka,” Ngilu alisema.

Kupitia kwenye ukuraa wake wa Facebook Jumamosi, Ngilu alisema hawatamruhusu Ruto kuja Ukambani na kumtusi kiongozi wao mwadilifu.

"...kama vile alivyofanya huko Meru akiwa na Gavana Kiraitu Murungi tukitazama. Haitajirudia," alisema.

"Ajiangalie, tofauti ya umri kati yao ieleweke kuwa hatakiwi kumtukana Kalonzo ambaye amekuwa uongozini kwa muda mrefu."

Ngilu alisema tofauti kati ya viongozi hao wawili ni kwamba Kalonzo ni mwaminifu na mtu mwingine sio.

"Kalonzo anategemewa sana na amejitahidi sana kuleta amani, ukimlinganisha yeye na Ruto ni kama usiku na mchana. Kalonzo anajaribiwa, sio jina la kucheza nalo. Huwezi kuja Ukambani kuongea vibaya. ya mtu wa Kalonzo," alisema.

Wiki iliyopita, Ruto alimweleza Kalonzo.

"Mimi sina shida na mtu yeyote, nilisaida Raila hadi akawa Waziri Mkuu lakini ilifika wakati nikagundua hapendi Mungu nikachoka nikamwachia Kalonzo," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved