Likionekana kama umbo la mraba, na mkato laini unaoonekana katika mwamba mkali, umbo la kijiolojia lililotengenezwa katika sayari ya Mars limeibua maswali kwa siku kadhaa.
Baadhi wamebaini kuwa ni umbo la "mlango" na wengine wameibuka na nadharia kuhusu iwapo ’’mlango’’ huu uliopo nje ya dunia unaweza kubuni "njia " ya kuingia katika sayari jirani.
Lakini kile kilichoonyeshwa ni picha iliyopigwa na roboti ya udadisi, ambayo imekuwa ikituma taarifa kuhusu sayari ya Mars kutoka duniani tangu mwaka 2012, ina maelezo zaidi ya kimantiki.
Kulingana na NASA, ni suala la kimtazamo.
NASA ilitambua picha kama sehemu ya msururu wa "Sol 3466" ambao ulichapishwa katika picha nyingi katika wavuti wa mpango wa uvumbuzi wa roboti
Baada ya kuchapishwa, baadhi ya watu mtandaoni walianza kuzungumzia nadharia kuhusu umbo lake na jinsi umbo hivyo lilivyo na muonekano wa ‘’mlango’’ au "njia"
Katika picha hii unaweza kuona mkusanyiko wa picha za misururu ya 3466 na jinsi umbo linavyoonekana kwenye mwamba wa Jezero , ambalo limevumbuliwa na roboti yenye udadisi katika wiki za hivi karibuni.