logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Aliniambia anauza tiketi za ndege- Babake Obegi akiri mwanawe alidanganya kuhusu kazi yake

Baba Obegi alifichua kuwa hakujua chanzo halisi cha mapato ya mwanawe.

image
na

Habari22 June 2022 - 10:57

Muhtasari


•Babake Obegi alieleza kwamba alifahamu kuhusu kifo cha mwanawe kupitia kwa mmoja wa marafiki zake.

•Mwili wa marehemu Obegi ulipatikana pamoja na ya Fred Obare, Elijah Omeka na Moses Nyachae katika Msitu wa Kijabe na eneo la Magadi.

Marehemu Frank Obegi katika picha ya faili Picha: Twitter

Babake marehemu Frank Obegi alizungumza na vyombo vya habari siku moja baada ya mwili wa mwanawe uliokuwa umekatwakatwa kupatikana katika Msitu wa Kijabe pamoja na miili ya wengine watatu.

Babake Obegi, Evans Bowendo, alieleza kwamba alifahamu kuhusu kifo cha mwanawe kupitia kwa mmoja wa marafiki zake. .

Isitoshe, Bw. Bowendo pia na mara zote alidhani aliuza ‘tiketi za ndege’ na kufanya uandishi wa kitaaluma.

“Nilidhani kuwa mwanangu aliuza tikiti za ndege mtandaoni. Hivyo ndivyo alivyokuwa ameniambia alipoondoka nyumbani Februari. Lakini sasa amekutwa amekufa, pia nimeshtuka ni kitu gani kilimfanya mwanangu afe  vile.

Alikuwa na pesa. Alipopata pesa ungeona kwenye status yake ya WhatsApp, mara Mombasa, wakati mwingine alikuwa kwenye ndege. Nilimuuliza akaniambia pesa alizonazo huwa ni yake kutokana na biashara aliyokuwa anaifanya'' Bw, Bowedo alisema.

Kaka yake Obegi kwa upande wake aliwaambia waandishi wa habari kwamba kwa sababu marehemu alikuwa mwanablogu maarufu, hakuwahi kutilia shaka chanzo cha mapato yake.

"Alikuwa mtu ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye mitandao ya kijamii, alikuwa mwanablogu, na labda alikuwa mahali pasipofaa, kwa wakati mbaya na watu wasiofaa."

Mwili wa marehemu Obegi uliokuwa na ishara za mateso ulipatikana pamoja na miili ya Fred Obare, Elijah Omeka na Moses Nyachae katika Msitu wa Kijabe na eneo la Magadi.

Wanne hao waliishi maisha ya kifahari wakizunguka nchi nzima kupitia ndege na matumizi yao ya kifahari katika vilabu na vituo mbalimbali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved