logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hisia mseto baada ya Sankok kutangaza kustaafu kutoka kwa siasa

Alibainisha kuwa alianza kupigania haki za watu wanaoishi na ulemavu akiwa na umri mdogo

image
na Radio Jambo

Habari04 July 2022 - 14:00

Muhtasari


  • Hisia mseto baada ya Sankok kutangaza kustaafu kutoka kwa siasa

Mbunge mteule David Sankok Jumatatu alitangaza kuwa anastaafu kutoka kwa siasa,huku akiibua hisia mseto mitandaoni.

Akizungumza katika mahojiano katika Spice FM, Sankok alisema hatafuti kiti chochote cha kuchaguliwa katika uchaguzi ujao wa Agosti kwani anataka kuangazia biashara za kibinafsi.

“Suala la kugombea ni uamuzi wa mtu binafsi. Niliamua wakati huu kutotafuta nafasi yoyote ya kuchaguliwa. Ninahitaji kuzingatia biashara zangu," alisema.

Alibainisha kuwa alianza kupigania haki za watu wanaoishi na ulemavu akiwa na umri mdogo na hakuwahi kupata nafasi ya kukuza biashara zake.

Sankok, mfuasi wa UDA, alipanda jukwaani kuunga mkono manifesto ya Naibu Rais William Ruto, akiwahimiza Wakenya kupiga kura kwa busara katika Uchaguzi Mkuu wa Agosti 9.

Sankok alisema hapo awali kuwa tangu kuteuliwa kwake katika Bunge la Kitaifa mwaka wa 2017, siasa zimemletea hasara kubwa ya kifedha.

Habari za kustaafu kwake ziliibua hisia mseto mitandaoni.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved