logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamume kamili hafai kuwa na Instagram, TikTok na Snapchat - Anerlisa Muigai

Muigai aliwataka wanaume kujitahidi na kutqafuta pesa ili kujizolea heshima kutoka kwa wanawake.

image
na Radio Jambo

Habari30 March 2023 - 07:21

Muhtasari


• Wanaume wanaopatikana kwenye mitandao ya kijamii, kulingana na Muigqai ni wale ambao hawana uhakika katika maisha.

Muigai afichua siri ya kutambua mwanamume kamili.

Mjasiriamali na mrithi wa kampuni ya vileo ya Keroche Anerlisa Muigai ameibuka na jipya kuhusu kigezo cha kutathmini wanaume kamili na wanaume magumegume.

Kwa mujibu wa mfanyibiashara huyo, mwanamume kamili ambaye ana utimamu wa kufurahia maisha kwa kujizolea utajiri na afya nzuri na kukimu familia vizuri, mwanamume huyo hafai kujipata au kupatikana katika mitandao ya kijamii hata kidogo.

Muigai anahisi kwamba mwanamume ambaye ako katika mitandao ya kijamii haswa haswa Instagram, TikTok na Snapchat, huyo si mwanamume wa kutegemewa kuwa atakuza familia au hata kujikuza mwenyewe.

Muigai alisema kwamba mwanamume kamili kama itabidi yeye kupatikana mitandaoni basi huwa ni mchache sana kwani muda mwingi hayuko kule bali anajishughulisha na masuala ya kumletea tija maishani.

“Mwanamume kamili hawezi kuwa na Instagram, Snapchat na TikTok kwa wakati mmoja. Wanaume kamili wa ukweli kabisa huwa hawapatikani kwenye mitandao ya kijamii. Na kama wanapatikana huko, basi huwa hawaitumii mitandao hiyo muda wote, angalau asilimia kubwa yao,” Muigai alisema.

Hii si mara ya kwanza kwa mrithi huyo wa Keroche kuibua vigezo vya kuwatambua wanaume kamili.

Wiki jana, Muigai kupitia instastory yake aliibua kigezo kingine akiashiria kwamba hakuna mwanamke anayepata furaha ubavuni mwa mwanamume maskini.

Muigai alipakia video iliyomuonesha mwanamume akiigiza kama mfumo wa kutoa pesa wa ATM huku mwanamke akimbofya kifuani kabla ya mwanamume huyo kuchomoza bunda la noti na kumkabidhi mwanamke aliyeng’aa kwa tabasamu pana usoni.

Muigai alisema furaha ya kila mwanamke ni mwanamume mwenye pesa, na kuwataka wanaume waache kujilaza kizembe na badala yake kutafuta hela kwa namna zote.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved