logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Lulu Hassan ammiminia sifa Rashid Abdalla siku yake ya kuzaliwa

Lulu Hassan alisema Rashid ana umuhimu mkubwa katika maisha yake.

image
na

Habari17 April 2023 - 11:08

Muhtasari


• Rashid Abdalla na Lulu Hassan ni wanandoa na wana watoto 3 pamoja.

Lulu Hassan amtakia kheir ya kuzaliwa mumewe, Rashid Abdalla.

Mtangazaji Lulu Hassan amwemwandikia mumewe   Rashid Abdalla maneno ya sifa katika siku yake ya kuzaliwa .

Lulu Hassan pia ni mtangazaji mwenza wa Rashid Abdalla katika programu ya Nipashe. Katika ukurasa wake wa Instagram, Lulu Hassan alieleza kuwa Rashid ana umuhimu sana katika maisha yake na kwamba ndiye kama baba ambaye hakufanikiwa kupata.

"Happy birthday mtu wangu,bosi wangu, baba ya watoto wangu. Mungu akupe umri mrefu na afya njema , wewe ni wa maana sana kwa maisha yangu, Mungu anajua. Wewe ni kama baba ambaye sikuwa naye rafiki yangu na mtu wangu. Mungu akulinde Rash, akupe hitaji la moyo na dua zako ndani ya mwezi huu mtukufu," alichapisha Lulu Hassan.

Rashid Abdalla alisherehekea siku yake ya kuzaliwa  siku ya Jumatatu.

"Mwenyezi Mungu nakuomba  uwape ufanisi wa kupitiliza, afya njema na ngekewa.Kwani wote wamekuwa nguzo muhimu katika maisha yangu. Kheir ya kuzaliwa kwangu," alisema Rashid

Lulu Hassan na Rashid Abdalla ni watangazaji wa runinga ya Citizen .Wawili hao ni wanandoa na wamebarikiwa na watoto watatu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved