logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mfuasi wa Pasta Mackenzie afariki kizuizini baada ya kugoma kula na kunywa kwa siku 10

Mchungaji Paul Mackenzi anazuiliwa na atafunguliwa mashtaka ya mauaji y halaiki.

image
na Davis Ojiambo

Habari21 June 2023 - 11:07

Muhtasari


  • • Mtu huyo aliyefariki alitajwa kwa jina Juma Joseph Buyuka na alikuwa miongoni mwa watu 30 ambao walikuwa wamehamishwa kwenda gerezani.
wafuasi wa Mackenzie wafikishwa mahakamani na kufunguliwa mashtaka ya kugoma kula.

Mtu mmoja anayedhaniwa kuwa mfuasi wa mhubiri tata Paul Mackenzie ameripotiwa kufariki akiwa katka kizuizi cha polisi baada ya kile kilitajwa kuwa ni njaa ya siku kumi.

Jarida la Nation liliripoti kwamba wengine wawili walikimbizwa hospitali wakiwa katika hali mbaya ya afya.

“Tunashuku marehemu alifariki kutokana na njaa ya chakula. Kwa sasa tusubiri tu uchunguzi wa maiti ili kubaini chanzo cha kifo,” mwendesha mashtaka aliiambia mahakama kama alivyonukuliwa na jarida la Nation.

Mtu huyo aliyefariki alitajwa kwa jina Juma Joseph Buyuka na alikuwa miongoni mwa watu 30 ambao walikuwa wamehamishwa kwenda gerezani baada ya kuanzisha mgomo wa kutokula wakiwa kwenye seli.

Mahakama iliambiwa kwamba marehemu alipelekwa katika hospitali ya Malindi baada ya afya yake kudhoofika akiwa gerezani.

Wiki jana watu hao walifikishwa mahakamani wakiwa katika hali ya kutia huruma ambapo mahakama ilisema wahamishiwe magereza na kuwekwa chini ya mpango wa kulazimishiwa chakula ili kuimarisha hali yao kabla ya kushtakiwa.

Kudikia sasa, shughuli ya ufukuaji maiti ambayo imesitishwa wiki jana imeona maiti Zaidi ya 300 ikifukuliwa katika shamba la Shakahola.

Mchungaji Paul Mackenzi anazuiliwa na atafunguliwa mashtaka ya mauaji y halaiki.

Waumini hao wengi ambao walifariki na miili yao kufanyiwa uchunguzi baada ya kufukuliwa ilionyesha dalili za kufa kutokana na kukosa chakula na maji.

Mackenzie anaarifiwa kuwataka waumini wake kujitesa hadi kufa kama njia moja ya kuwapa uhakikisho wa kukutana na Yesu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved