Seneta Boni halwale afanya upasuaji wa masaa mawili kuokoa maisha ya mhadhiri

Kulingana na picha alizoshiriki Khalwale, Lidigu alijeruhiwa mara kadhaa kichwani na mkononi.

Muhtasari

•Khalwale alisema mgonjwa wake, mhadhiri wa Kisumu Polytechnic Sebastian Lidigu alijeruhiwa vibaya kwa panga baada ya mwanawe kumshambulia.

•Khalwale alisomea udaktari katika Chuo Kikuu cha Nairobi kuanzia 1980 hadi 1987, na kuhitimu Shahada ya Udaktari na Shahada ya Upasuaji.

katika wadi ya Hospitali ya Mukumu mnamo Juni 24,2023.
Seneta wa Kakamega Boni Khalwale katika wadi ya Hospitali ya Mukumu mnamo Juni 24,2023.
Image: HISANI

Jumamosi haikuwa siku ya kawaida ofisini kwa Seneta wa Kakamega Boni Khalwale baada ya kuombwa kufika katika hospitali ya Mukumu kufanya upasuaji.

Katika taarifa, Khalwale alisema mgonjwa wake, mhadhiri wa Kisumu Polytechnic Sebastian Lidigu alijeruhiwa vibaya kwa panga baada ya mwanawe kumshambulia.

Seneta huyo hata hivyo alifika kwa wakati katika Hospitali ya Mukumu na kumfanyia upasuaji wa masaa mawili.

"Mhadhiri wa Kisumu Polytechnic Sebastian Lidigu alijeruhiwa vibaya leo asubuhi baada ya mwanawe wa kuchomelea panga kumvamia. Nimefurahi kuokoa maisha yake baada ya operesheni kali ya masaa mawili na dakika 10 katika Hospitali ya Mukumu," alisema.

Kulingana na picha alizoshiriki Khalwale, Lidigu alijeruhiwa mara kadhaa kichwani na mkononi.

Bado haijafahamika ni nini kilisababisha shambulio hilo.

Kabla ya siasa, Khalwale alihudumu kama daktari.

Alisomea udaktari katika Chuo Kikuu cha Nairobi kuanzia 1980 hadi 1987, na kuhitimu Shahada ya Udaktari na Shahada ya Upasuaji.

Alitumwa kama afisa wa matibabu jijini Nairobi katika Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta, wilaya za Kakamega, Kisii, Machakos, Msambwebi na Kirinyaga.

Alisema uzoefu wake wa kwanza katika usimamizi ulikuwa kati ya 1988-90 katika iliyokuwa Wilaya ya Kakamega (sasa kaunti ya Kakamega) ambapo anajivunia kuhakikisha kuwa hospitali zote, vituo vya afya na zahanati zinafanya kazi ipasavyo zikiwa na wahudumu wa kutosha, usambazaji wa dawa na chanjo kila mara.

Baadaye, alifanya kazi kibinafsi katika miji ya Mombasa na Kakamega kutoka ambapo alijiunga na siasa za kitaifa.

Katika shughuli za kawaida za kila siku, seneta anatarajiwa kuwakilisha masilahi ya kaunti.

Katika Seneti, wanashiriki katika utungaji sheria kwa kuzingatia, kujadili na kuidhinisha miswada inayohusu kaunti.

Pia huamua mgao wa mapato ya kitaifa kati ya kaunti