logo

NOW ON AIR

Listen in Live

William Ruto amekuwa crush wangu tangu kitambo akiwa MP - Sandra Dacha

“William Ruto kusema ukweli umekuwa crush wangu wa muda mrefu, tangu enzi zile ukiwa Mbunge,”.

image
na Radio Jambo

Habari03 August 2023 - 07:46

Muhtasari


• "Zakayo amekuwa crush wangu kutoka kitambo hiyo lakini wakati mwingine nabadilisha mawazo yangu,” alisema.

Sandra Dacha.

Muigizaji Sandra Dacha amekiri kwamba rais William Ruto ndiye mtu mashuhuri ambaye ni crush wake.

Dacha alisema haya wakati wa mazungmzo na mchekeshaji Oga Obinna kwenye kipindi cha KulaCooler kwenye chaneli yake ya YouTube.

Mchekeshaji huyo ambaye hajawahi ona aibu kutokana na watu kuwadhihaki watu mitandaoni, alifunguka kwamba hajaanza kuwa na crush wa rais Ruto hivi majuzi bali ni kutoka kitambo kiongozi huyo alipokuwa mbunge wa Eldoret Kaskazini.

“Ruto, William. Naapa ni yeye. Tangu kitambo akiwa mbunge. Zakayo amekuwa crush wangu kutoka kitambo hiyo lakini wakati mwingine nabadilisha mawazo yangu,” alisema.

Obinna aliwambia kuchukua fursa hiyo kumuambia rais jambo moja, pengine atatazama kipindi hicho, akimsisitizia kwamba huenda hiyo ikawa ni fursa yake ya kuvuka mstari kutoka maisha ya kawaida kwenda maisha ya ukwasi.

“William Ruto kusema ukweli umekuwa crush wangu wa muda mrefu, tangu enzi zile ukiwa Mbunge,” alitoa neno kwa Ruto.

Kwa mara ya kwanza, muigizaji huyo ambaye pia ni mchekeshaji alisema kwamba mara ya kwanza walikutana na Akuku Danger ilikuwa ni katika mazishi ya mcheshi marehemu Othuol Othuol miaka michache iliyopita.

Mama huyo wa mtoto mmoja alisema kwamba anatarajia kumzalia Akuku mtoto pindi tu watakapofunga harusi.

Hata hivyo, uhusiano wake na Akuku, ambaye pia anasemekana kuwa na familia umekuwa ukichukuliwa kimzaha wengi wakihisi ni wa mitandaoni tu lakini katika uhalisia wa maisha ni marafiki tu.

Kwa upande wao, Sandra na Akuku wamekuwa wakisisitiza kwamba wao ni wapenzi na watafunga harusi hivi karibuni.

Sandra aliweka wazi kwamba yeye na Akuku ni mtu na mpenzi wake mwaka jana wakati alikuwa anaongoza kampeni ya kuchangisha pesa mitandaoni ili kugharamia matibabu ya Akuku Danger ambaye anaugua ugonjwa wa Seli Mundu.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved