logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tazama matukio kuhusu mlipuko wa gesi Embakasi kufikia Jumanne

Mfanyibiashara anayeaminika kuwa mmiliki wa eneo hilo haramu la kujaza gesi ni miongoni mwa wale ambao wamekamatwa.

image
na SAMUEL MAINA

Habari07 February 2024 - 04:22

Muhtasari


  • •Mfanyibiashara anayeaminika kuwa mmiliki wa eneo hilo haramu la kujaza gesi ni miongoni mwa wale ambao wamekamatwa.
  • •Baadhi ya waathiriwa walitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani huku wengine wakiwa bado wamelazwa katika hospitali mbalimbali.
kuhusu mlipuko wa gesi Embakasi.

Kurugenzi ya Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI) inaendelea na uchunguzi kuhusu kisa cha mlipuko hatari wa gesi uliotokea katika mtaa wa Embakasi, Nairobi mnamo Februari 1, 2024, na kuua watu watatu papo hapo na kuwaacha wengine wengi na majeraha tofauti.

Katika ripoti ya Jumanne asubuhi, Februari 6, wapelelezi walifichua kuwa kufikia sasa, watu wanne wamekamatwa na kuwekwa chini ya ulinzi kuhusiana na tukio hilo la kusikitisha.

Mfanyibiashara anayeaminika kuwa mmiliki wa eneo hilo haramu la kujaza gesi, Derrick Kimathi ni miongoni mwa wale ambao wamekamatwa. Maafisa watatu wa NEMA pia wako kizuizini.

Idara ya DCI inaendelea na msako wa washukiwa wengine watano waliohusishwa na tukio hilo la mapema Februari ambao wanaripotiwa kuwa mafichoni

Kufikia sasa, waathiriwa sita wa mlipuko huo mbaya wa gesi wamefariki huku watu wengine wapatao mia tatu wakiripotiwa kujeruhiwa kwa viwango tofauti vya moto.

Baadhi ya waathiriwa walitibiwa na kuruhusiwa kwenda nyumbani huku wengine wakiwa bado wamelazwa katika hospitali mbalimbali wakiwa katika hali tofauti.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved