logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uvumi waibuka kuwa Hassan Mugambi na Chumutai Goin wamepata kazi serikalini

Mugambi anadaiwa kuondoka mwezi Machi kufanya kazi katika afisi ya waziri Aden Duale.

image
na Davis Ojiambo

Habari14 February 2024 - 14:57

Muhtasari


  • Mugambi baada ya kuhama runinga ya K24 alijiunga Citizen TV mwaka wa 2016  Septemba kama ripota wa Kiswahili. 
  • Chemutai Goin pia alituzwa na rais katika sherehe za Madaraka  mwaka wa 2020.

Wanasema penye moshi hapakosi moto, uvumi umezuka mitandaoni kuwa mwanahabari tajika Hassan Mugambi huenda yuko njiani kuondoka Citizen TV.

Kulingana na duru karibu na mwanahabari huyo, anapanga kuondoka Citizen mwezi Machi kwenda kufanya kazi katika afisi ya waziri wa Ulinzi, Aden Duale.

Mwanahabari mwenzake Chemutai Goin pia inadaiwa ataondoka mwezi Machi kujiunga na ofisi ya Spika wa bunge la kitaifa Moses Wetang'ula.

Uvumi huu umezua mjadala mtandaoni wengine wakisema kuwa wata'miss wanahabari hao, huku wengine wakisema kuwa serikali inachukua wanahabari wote wazuri kama Hussein Mohammed na Kanze Dena.

Mugambi baada ya kuhama runinga ya K24 alijiunga Citizen TV mwaka wa 2016  Septemba kama ripota wa Kiswahili. 

Chemutai Goin alifanya kazi kwa radio kabla ya kuenda runinga kama ripota wa siasa. 

Chemutai Goin pia alituzwa na rais katika sherehe za Madaraka  mwaka wa 2020.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved