logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msichana apandwa na hasira huku babake akinyoa nywele zake kwa siri akiwa amelala

Hata hivyo, hakufichua sababu ya uamuzi wa baba yake zaidi ya kuumia kwake.

image
na Radio Jambo

Habari21 February 2024 - 06:01

Muhtasari


• “Baada ya kujua baba alinichafua kwa kunikata nywele. Ingawa nililia sana, nina imani kidogo,” alinukuu video hiyo.

Binti mmoja wa Afrika Kusini anaonyesha hasira na masikitiko makubwa baada ya kuamka na kukuta baba yake alimfanyia kitendo ambacho hakuna msichana wa umri wa balehe anaweza tabasamu nacho.

Mrembo huyo katika video alisema kwamba aliamka kutoka usingizini na kupata shungi la nywele zake kichwani hazimo ni upara tu na kwa kuuliza akaambiwa ni babake alimfanyia hivyo.

Watumiaji wa mitandao ya kijamii walichanganyikiwa na ufichuzi wa msichana mdogo wa jinsi babake alikuwa amekata nywele zake zote bila kutarajia alipokuwa amelala.

Katika video ya TikTok iliyoshirikiwa na @somilamashiqa, alionyesha kusikitishwa kwake kwa kutawanyika chumba chake kuguswa na tukio hilo.

Katika video iliyofuata, alifichua muonekano wake uliobadilika na kukiri kwamba ilikuwa imeathiri sana kujiamini kwake. Hata hivyo, hakufichua sababu ya uamuzi wa baba yake zaidi ya kuumia kwake.

“Baada ya kujua baba alinichafua kwa kunikata nywele. Ingawa nililia sana, nina imani kidogo,” alinukuu video hiyo.

Video hiyo tangu wakati huo imezua wimbi la hisia kutoka kwa watumiaji wa mitandao ya kijamii ambao wanaweza kuhusiana na kutendewa sawa na wazazi wao, haswa baba yao huku wengine wakilaani kitendo hicho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved