logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto amzomea Mbunge Peter Salasya kwa kutochana nywele zake

Ruto aliendelea na mazungumzo akimuuliza kwa nini hakuwa amechana nywele zake.

image
na SAMUEL MAINA

Habari21 March 2024 - 09:01

Muhtasari


  • •Rais aliwafanya viongozi wengine kuangua kicheko kikubwa alipomuuliza mbunge huyo wa muhula wa kwanza sababu iliyomfanya asichane nywele.
  • •Ruto aliendelea na mazungumzo akimuuliza kwa nini hakuwa amechana nywele zake.
akisalimiana na Mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya alipowasili Kakamega kufungua Kongamano la Kimataifa la Uwekezaji la Kaunti mnamo Machi 20, 2024.

Video inayoonyesha rais William Ruto akimfanyia mzaha mbunge wa Mumias Mashariki Peter Salasya kuhusu nywele zake zilizochanika imesambaa sana kwenye mitandao ya kijamii.

Katika video hiyo iliyorekodiwa Kakamega siku ya Jumatano, rais aliwafanya viongozi wengine kuangua kicheko kikubwa alipomuuliza mbunge huyo wa muhula wa kwanza sababu iliyomfanya asichane nywele zake.

Rais alikuwa akiwasalimu viongozi  wengine alipowasili Kakamega kufungua Kongamano la Kimataifa la Uwekezaji la Kaunti ya Kakamega wakati  alipokutana na Salasya.

Wabunge wa Bunge la Kitaifa na Seneti walikuwa wamejipanga kumkaribisha Rais katika kaunti hiyo ya Maghabribi mwa Kenya.

Huku akiwasalimia kwa mkono viongozi hao, aliwaita kwa majina akiuliza jinsi maeneo ambayo wanawakilisha yanaendelea.

Hatimaye zamu ya ,bunge Peter Salasya ilifika, na alionekana kuwa na shauku ya kumsalimia kiongozi huyo wa taifa.

Mbunge huyo wa Mumias Mashariki alimpa rais mikono yake kwa nguvu huku akiegemeza macho yake moja kwa moja kwa kamera.

Rais alimuuliza anaendeleaje na akamjibu anaendelea vizuri huku akiwa na tabasamu kubwa.

Jibu lake likapelekea viongozi wengine kuangua vicheko.

Ruto aliendelea na mazungumzo akimuuliza kwa nini hakuwa amechana nywele zake.

“Mbona haujachanua nywele,” Rais aliuliza.

Mbunge akajibu kwa mbwembwe nyingi alijibu "Ukisema nitachanua".

Jibu lake lilipelekea Rais na wengine waliokuwepo kuangua kicheko.

Mbunge huyo wa muhula wa kwanza anajulikana kwa staili yake ya nywele ndefu kidogo ambayo aghalabu huwa hachani.

Rais Ruto alifungua rasmi Kongamano la Kimataifa la Uwekezaji la Kaunti ya Kakamega mnamo siku ya Jumatano.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved