logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Unanipenda au unanitumia tu?” Zuchu amuuliza Diamond, ataka kujua ndoa ni lini (video)

“Unanipenda mimi? Utanioa lini? Au unanitumia?” Zuchu alimuuliza Diamond.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku17 April 2024 - 07:10

Muhtasari


• Moja kati ya tumbuizo lililozua gumzo Zaidi mitandaoni ni pale Zuchu na Diamond walipopanda jukwaani kwa ajili ya kutumbuiza wimbo wao wa pamoja ‘Mtasubiri sana’.

• Wakati huo huo, Diamond naye alimuimbia akimuuliza maswali hay ohayo na pia kutaka kujua Zuchu atamzalia lini.

Diaond na Zuchu kwenye ubora wao jukwaani.

Usiku wa Jumanne, asilimia kubwa ya wasanii wa Tanzania walijumuika katika mkoa wa Tanga wilayani Pangani kwa ajili ya Mkesha wa Mwenge.

Katika hafla hiyo ya tafrija, wasanii mbalimbali walipanda jukwaani na kuwatumbuizia mashabiki kwa nyimbo zao pendwa.

Moja kati ya tumbuizo lililozua gumzo Zaidi mitandaoni ni pale Zuchu na Diamond walipopanda jukwaani kwa ajili ya kutumbuiza wimbo wao wa pamoja ‘Mtasubiri sana’.

Katika wimbo huo ambao upo kama shiri la ngonjera, wawili hao ambao pia wamekuwa wakitajwa kama wapenzi waliimbiana kwa zamu mistari ya kuulizana maswali kuhusu mapenzi yao.

Zuchu aliushangaza umati baada ya kuchombeza maneno yake ya kibunifu akimuuliza Diamond kama anampenda kweli na pia kwenda ndani Zaidi akitaka kujua ni lini Diamond atamuoa rasmi kwa ndoa ya Nikkah.

Wakati huo huo, Diamond naye alimuimbia akimuuliza maswali hay ohayo na pia kutaka kujua Zuchu atamzalia lini.

“Unanipenda mimi? Utanioa lini? Au unanitumia?” Zuchu alimuuliza Diamond.

 “Unanipenda mimi? Unaniamini? Utanizalia lini?” Diamond alimjibu Zuchu kwa kutumia maswali pia.

Kufuatia maswali yake ya kijanja, mashabiki waliohudhuria hafla hiyo walifurahishwa na walionekana kumuunga Zuchu mkono kwa swali lake kwa Diamond kuhusu ndoa.

Walifanya kama kiitikio wakiradidi “Muoe! Muoe! Muoe!” huku Zuchu akiwarushia noti za pesa kutoka jukwaani.

Wakiwa wapenzi, wawili hao bado hawajafunga ndoa licha ya tetesi kutoka kwa wazazi wao kudai wawili hao wanachezea saikolojia za mashabiki tu.

Hii hapa video ya Zuchu na Diamond jukwaani kwenye mkesha wa Mwenge, Pangani, mkoa wa Tanga:

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved