logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila Odinga aomboleza kifo cha Jenerali Francis Ogolla

Moses Wetangula, Spika wa Bunge la Kitaifa pia aliungana na taifa kuomboleza msiba wa CDF Ogolla.

image
na Davis Ojiambo

Habari19 April 2024 - 06:34

Muhtasari


  • Jenerali Ogolla, pamoja na wanajeshi wengine kumi na moja, walihusika katika ajali mbaya ya helikopta katika eneo la Sindar, eneo la Kaben huko Elgeyo Marakwet, ambayo ilileta taharuki kote nchini

Kiongozi wa upinzani Raila Odinga ameelezea kusikitishwa kwake na kifo cha Jenerali Francis Omondi Ogolla, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, aliyepoteza maisha katika ajali ya helikopta.

Jenerali Ogolla, pamoja na wanajeshi wengine kumi na moja, walihusika katika ajali mbaya ya helikopta katika eneo la Sindar, eneo la Kaben huko Elgeyo Marakwet, ambayo ilileta taharuki kote nchini.

Katikaheshima yake kwa Jenerali Ogolla, Raila Odinga alisema: “Siku mbaya kwa Kenya: Mke wangu Ida na mimi tumehuzunishwa sana na kifo cha Jenerali Francis Ogolla, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi."

Akiongeza, “Tunaungana na taifa katika kuomboleza kifo chake. Jenerali Ogolla alikuwa mzalendo wa kweli, mwanajeshi aliyepambwa sana na mtaalamu aliyekamilika ambaye alitumikia nchi yetu kwa kujitolea bila kuyumbayumba.”

Akielezea mshikamano na familia iliyojawa na huzuni, Raila aliongeza: “Mioyo yetu ni kwa familia yake, wafanyakazi wenzake katika KDF na taifa zima tunapoomboleza kifo huu mkubwa. Pia tunatuma rambirambi zetu kwa familia za timu ya KDF iliyoandamana na Jenerali Ogolla. Tunajua kwamba kwa wakati huu, maneno hayatatosha kufariji huzuni zenu kubwa. Tunawaombea Bwana awafariji na roho za wote waliofariki zipate amani ya milele.”

 

Moses Wetangula, Spika wa Bunge la Kitaifa pia aliungana na taifa kuomboleza msiba wa CDF Ogolla.

Katika heshima kubwa, Spika Wetangula alielezea masikitiko yake makubwa kutokana na kufariki kwa Jenerali Ogolla na maafisa wenzake ambao utumishi wao wa kujitolea kwa taifa utakumbukwa kwa taadhima.

“Nasimama pamoja na taifa na vikosi vyetu vilivyo na nidhamu katika kuomboleza msiba wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Francis .O. Ogolla, ambaye alifariki katika ajali ya helikopta akiwa kazini katika Wilaya ya Elgeiyo Marakwet inalemea mioyo yetu,” alisema Spika Wetangula.

Spika Wetangula amewatakia manusura wa ajali hiyo ahueni ya haraka na kuomba dua ili roho za marehemu zipate amani ya milele.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved