logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Binti mfalme wa Dubai atangaza kumtaliki mume wake kupitia Instagram

Binti wa mtawala wa Dubai ametangaza kumtalaki mume wake kupitia mtandao ya kijamii.

image
na SAMUEL MAINA

Habari18 July 2024 - 11:16

Muhtasari


  • •Ujumbe kutoka kwa Instagram iliyothibitishwa ya Sheikha Mahra bint Mohammed bin Rashid Al Maktoum ulisema anakatisha ndoa yake kwa kuandika: "Mimi natangaza talaka yetu."

Binti wa mtawala wa Dubai ametangaza kumtalaki mume wake kupitia mtandao ya kijamii.

Ujumbe kutoka kwa akaunti ya Instagram iliyothibitishwa ya Sheikha Mahra bint Mohammed bin Rashid Al Maktoum ulisema anakatisha ndoa yake kwa kuandika: "Mimi natangaza talaka yetu."

BBC imewasiliana na maafisa nchini humo ili kupata ufafanuzi kuhusu suala hilo.

Hadi kufikia sasa, sio mume wake Sheikha Mahra, Sheikh Mana bin Mohammed bin Rashid bin Mana Al Maktoum, wala baba yake, ambaye ametoa maoni kuhusu suala hilo kwa umma.

Ujumbe huo, ambao ulianza kwa kusema "Mume wangu Mpendwa", ulihitimishwa na maneno - "Ninakupa talaka, ninakupa talaka, na ninakupa talaka," ukionekana kutumia desturi ya Kiislamu inayojulikana kama talaka tatu.

Kitendo hicho kimepigwa marufuku katika nchi nyingi, lakini kwa kawaida huwaruhusu waume kuwataliki wake zao haraka kwa kusema “Ninakupa talaka” mara tatu.

"Kila la kheri. Mke wako wa zamani," ujumbe huo wa kwenye Instagram uliandikwa.

Picha zote za mume wa Sheikha Mahra zinaonekana kuwa zimefutwa kwenye akaunti yake.

Vile vile, akaunti ya Sheikh Mana inaonyesha picha za mke wake zimefutwa.

Wenzi hao walioana mnamo Aprili 2023 katika sherehe ya kifahari, na mtoto wao wa kwanza alizaliwa miezi miwili iliyopita.

Baadhi ya maoni kutoka kwa watumiaji wa Instagram wanakisia kuwa akaunti ya Sheikha Mahra inaweza kuwa imedukuliwa lakini hakujakuwa na dalili au usemi rasmi juu ya hilo.

Wakati ujumbe huo wa kumtalaki mume wake unaonekana ulionyesha kuwa umekuwepo kwa siku moja.

Serikali ya Dubai na Ubalozi wa UAE mjini London hawakujibu mara moja maombi ya kupata maoni yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved