logo

NOW ON AIR

Listen in Live

EACC yanasa mihuri bandia katika kesi ya ufisadi wa shilingi bilioni 1.6

Mihuri hiyo ilipatikana katika nyumba ya mshukiwa mmoja aliyoibadilisha kuwa ofisi

image
na Brandon Asiema

Habari29 October 2024 - 07:55

Muhtasari


  • Maafisa watendaji wa kamati za kaunti (CEC) ni baadhi ya washukiwa wakuu wa ufisadi katika sakata hiyo kwenye kaunti ya Bomet.
  • Mshukiwa mmoja yupo mafichoni baada ya EACC kufanya msako nyumbani kwake.

caption

Maafisa katika tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC wamepata mihuru 121 ya kampuni kadhaa za uhandis wa barabara katika kaunti ya Bomet.


Mihuri hiyo bandia inadaiwa kutumika katika kuendesha ufisadi wa takribani shilingi bilioni 1.6 katika madai yanayowausisha maafisa wa kamati ya utendaji wa kaunti CEC na maafisa wakuu waliokamatwa Alhamisi tarehe 24.


Katika uchunguzi wa EACC, maafisa walipata ofisi inayodaiwa kutengeneza stakabadhi bandia nyumbani kwa mhandisi Victor Kipkemoi Cheruiyot aliyetoroka na kuwaacha maafisa hao nyumbani wakati wa msako.


EACC inaamini kuwa mshukiwa huyo amekuwa akitengeneza stakabadhi bandia alizokuwa akitumia kudai malipo ya miradi isiyokuwepo kwa ujshirikiano na maafisa katika kaunti ya Bomet.


Nyumbani kwa Victor Kipkemoi, kulipatikana pia hati za ununuzi na malipo zilizodhibitishwa na maafisa wa kampuni mbali mbali pamoja na hnati za zabuni zinazosubiri kutiwa sahihi.


Vile vile, stakabadhi za maagizo ya ununuzi, hati za malipo ambazo hazijatumika pamoja na stakabadhi za mahitaji ya kazi mbali mbali za ujenzi kwa makampuni zinazoshukiwa kuwa ghushi zilipatikana nyumbani kwa mshukiwa huyo.


Aidha, EACC inaendelea kufanya uchunguzi wa washukiwa kupata mali ya umma kwa njia za udanganyifu.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved