logo

NOW ON AIR

Listen in Live

EACC yamchunguza meneja wa mamlaka ya bahari nchini kwa madai ya ufisadi

Meneja huyo anadaiwa kutoa zabuni kinyume cha sheria kwa kampuni ya bima ya matibabu

image
na Brandon Asiema

Habari01 December 2024 - 09:53

Muhtasari


  • Mwasaru alikamatwa katika operesheni ambayo pia ililenga kuwakamata  mawakala wawili wa bima wanaoaminika kuwa walishirikiana na meneja huyo kwenye kashfa hiyo ya bima.
  • EACC  inachunguza ununuzi wa bima ya matibabu ya wafanyakazi katika taasisi za umma ikidaiwa kuwa maafisa wengi wa serikali hutumia njia hiyo katika ubadhirifu wa fedha za umma.


Tume ya maadili na kupambana na ufisadi EACC inamchunguza meneja katika mamalaka ya bahari nchini kwa madai ya kuhusika na ufisadi wa shilingi 40,539,760 kupitia zabuni.

Maafisa wa EACC kwa waranti ya mahakama, walimkamata Henry Mwasaru  mnamo Jumanne Novemba 26, ambaye ni msimamizi wa wafanyakazi na utawala kwenye mamlaka ya KMA, kufuatia madai ya kuhusika katika ufisadi kwenye zabuni ya usamabazaji wa bima ya afya kwa wafanayakazi wa mamlaka hiyo.

Mwasaru alikamatwa katika operesheni ambayo pia ililenga kuwakamata  mawakala wawili wa bima wanaoaminika kuwa walishirikiana na meneja huyo kwenye kashfa hiyo ya bima.

Katika madai hayo, Mwasaru anakisiwa kushirikiana na mkuu wa usimamizi wa ugavi kwenye mamlaka hiyo Bevaline Lundu katika kutoa zabuni hiyo ya bima ya afya kwa kampuni moja ya bima kinyume cha sheria.

EACC imesema kwamba tayari imepata ushahidi muhimu ambao utawasaidia wakati wanaendelea na uchunguzi baada ya kuarifiwa mnamo Septemba 30, 2024 kwamba maafisa kadhaa katika mamlaka ya KMA walipeana zabuni kwa kampuni moja kinyume cha sheria.

EACC hata hivyo imesema kwamba inachunguza ununuzi wa bima ya matibabu ya wafanyakazi katika taasisi za umma ikidaiwa kuwa maafisa wengi wa serikali hutumia njia hiyo katika ubadhirifu wa fedha za umma.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved