Mwanahabari maarufu wa kimataifa kutoka Kenya Larry Madowo mnamo Jumapili jioni alikejeli maandishi ya kutambulisha Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kisumu.
Mwanahabari huyo wa CNN alikuwa akisafiri kwa kutumia uwanja huo wa ndege baada ya kushinda siku nzima mjini Kisumu alipotambua jinsi maandishi hayo yalivyomulikwa kwa sehemu tu.
Mwangaza uliomulika maandishi hayo iliwaka hadi “KISUMU INTERN” huku maandishi mengine “..ATIONAL AIRPORT” yakiwa hayawezi kuonekana vizuri kwa vile hayakuwa na mwanga.
Larry alichukua picha ya maandishi hayo na kuyafanyia mzaha akisema, "Usiku mwema kutoka Kisumu Intern."
Aliendelea kutania kuwa huenda uwanja huo wa ndege ulikuwa kwenye hali ya kuhifadhi nishati.
"Je, iko kwenye hali ya kuokoa nishati?" Alisema.
Tazama maoni ya baadhi ya Wakenya kwenye Facebook;
Anne Nyambura: Same thing at Moi International Airport,
Mombasa.
Kimutai.co.ke: Hiyo ni decoration, it lights on turns at an
interval of 1 hour, you could hang around kidogo and the remaining letters
could light up.
Solomon Muingi: Hii pia Adani aje kufix hiyo taa?
John Marenya: Our Kisumu intern is in training to be an international
airport in future.
Felix Oluoch Okoth: The rest of the letters are silent.
Katika miaka ya hivi majuzi, mwanahabari Larry Madowo amekuwa na sauti kubwa kukosoa hali ya viwanja vya ndege vya Kenya, haswa Uwanja wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA).
Mwaka huu na mwaka jana alilalamikia sana kuhusu kukatika kwa umeme na paa kuvuja kwenye uwanja huo wa ndege wa kimataifa, akitaka serikali kuboresha viwango