logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Vitambulisho 96 vyapatikana mikononi mwa mshukiwa wa ulaghai

Mshukiwa huyo anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Ruaraka wakati upelelezi zaidi ukiendelea.

image
na Brandon Asiema

Habari10 January 2025 - 09:51

Muhtasari


  • Kukamatwa kwa mshukiwa huyo kunajiri baada ya msako wa siku kadhaa uliondeshwa na maafisa wa usalama.
  • Jamaa huyo amekuwa akitumia vitambulisho vya kitaifa vya watu mbali mbali kusajili akaunti kadhaa kwenye jukwaa la biashara la mtandaoni.


Maafisa wa ujasusi wanamzuiliwa jamaa mmoja mwenye umri wa miaka 30, aliyepatikana na vitambulisho vya kitaifa vya watu vilivyopotea, simu 10 bandia na idadi ya maganda ya kuhifadhi laini za simu.

Kukamatwa kwa mshukiwa huyo kunajiri baada ya msako wa siku kadhaa uliondeshwa na maafisa wa usalama wakimtafuta mshukiwa huyo anayedaiwa kutekeleza wizi katika gari moja mnamo Januari 3.

Katika msako kwenye nyumba ya mwanamume huyo bidhaa hizo zilipatikana zikiwa chini ya umilisi wa mshukiwa katika mtaa wa Hilton viungani mwa eneo la Ruiru.

Uchunguzi wa maafisa wa polisi kupitia hojaji kwa mshukuwa umebaini kwamba jamaa huyo amekuwa akitumia vitambulisho vya kitaifa vya watu mbali mbali kusajili akaunti kadhaa kwenye jukwaa la biashara la mtandaoni.

Pia, ilibainika kuwa akaunti ghushi zinazosajiliwa na mshukiwa uyo hutumika kuwalaghai Wakenya mtandaoni kwa uwongo wa kuwauzia bidhaa za simu ambazo huwa ghushi.

Ulaghai unaoendeshwa na mshukiwa huyo ambaye sasa yuko mikononi mwa maafisa wa polisi, huwasababishia ukosefu wa amani watu wengine ambao kwa uhalisia hawakuhusika kwenye ulaghai bali ni vitambulisho vyao vilivyopotea hutumika kuendesha ulaghai huo.

Hata hivyo wapelelezi wanaamini kuwa walalamikaji zaidi waliokubali hila za mshukiwa wako nje, na wanaitwa kuripoti kituoni ili kurekodi kauli zao.

Mshukiwa huyo anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Ruaraka wakati upelelezi zaidi ukiendelea.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved