logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ichung’wah: Nitaendelea Kumtetea Rais Ruto Hata Wakisema Eti Mimi Ni Bibi Yake

“Nasikia huko kwa mitandao wananiita eti mimi ni bibi wa Ruto...Lakini hata wanitukane, mimi ukicheza na hii serikali, na huyu rais na naibu wake ni mimi na wewe mundu khu mundu.”

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari11 January 2025 - 13:56

Muhtasari


  • Ichung’wah alitoa tetesi zenye ukakasi mkubwa kwamba Natembeya alihusika katika utekaji nyara wa watu kipindi akiwa kama RC wa mkoa wa bonde la ufa.

  • “Huyo wa kutembea akikuja nitembee na yeye? Atembee asitembee? Na mmuambie mimi si mtu wa kutishwa,” Ichung’wah alisema.

MBUNGE wa Kikuyu ambaye pia ni kiongozi wa wengi katika bunge la kitaifa, Kimani Ichung’wah amesisitiza kwamba hakuna kauli cyoyote ya kumdunisha itamfanya kukoma kuendelea kumtetea rais William Ruto na serikali ya Kenya Kwanza.


Akizungumza katika bonde la ufa alipoandamana na rais katika ziara yake ya siku 3 ya kimaendeleo, mbunge huyo alisema kwamba baadhi ya watu wanatumiwa na wanasiasa kugawanya wananchi na kuzua chuki dhidi ya rais.


Ichung’wah alisema kwamba amesikia kwenye mitandao wanamuita ‘bibi ya rais’ lakini akasema hilo halitamfanya kuacha kutetea serikali ya Ruto na yeyote anamshambulia rais atapatana na yeye.


“Na mtu wa kucheza na rais Ruto, tunaangaliana macho kwa macho. Hata waseme eti mimi ni bibi ya rais, si nasikia huko kwa mitandao wananiita eti mimi ni bibi wa Ruto…si wanajua bibi wa mheshimiwa rais? Lakini hata wanitukane, mimi ukicheza na hii serikali, na huyu rais na naibu wake ni mimi na wewe mundu khu mundu,” Ichung’wah alisisitiza.


Aidha, mbunge huyo wa Kikuyu alirudha dongo kwa gavana wa Trans Nzoia George Natembeya baada ya kutishia kumchukulia hatua za kisheria kwa kauli aliyotoa dhidi yake wiki chache zilizopita katika hafla ya mazishi ya mamake spika wa bunge la kitaifa, Moses Wetang’ula.


Ichung’wah alitoa tetesi zenye ukakasi mkubwa kwamba Natembeya alihusika katika utekaji nyara wa watu kipindi akiwa kama RC wa mkoa wa bonde la ufa.


“Huyo wa kutembea akikuja nitembee na yeye? Atembee asitembee? Na mmuambie mimi si mtu wa kutishwa,” Ichung’wah alisema.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved