logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais Ruto Adai Wanasiasa Wanalipa Vijana Ili Kuweka Picha Za Viongozi Kwenye Majeneza

"Leo mtaweka viongozi kwenye kaburi kesho mtaweka wazazi wenu kwenye kaburi na keshokutwa mtaweka wenzenu, marafiki zenu," Ruto alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari11 January 2025 - 10:25

Muhtasari


  • "Leo mtaweka viongozi kwenye kaburi kesho mtaweka wazazi wenu kwenye kaburi na keshokutwa mtaweka wenzenu, marafiki zenu," Ruto alisema.
  • Mkuu wa taifa alisema kwamba kwa sasa vijana wa Kenya zaidi ya 120,000 wanatengeneza pesa kutoka kwa mitandao ya kijamii kutokana na matumizi mazuri ya mitandao hiyo.



RAIS WILLIAM Ruto sasa ameibuka na madai mapya kuhusu mwenendo wa baadhi ya vijana wanaotumia mitandao ya kijamii kutengeneza picha za baadhi ya viongozi kwenye majeneza na makaburi.


Akizungumza wakati wa kuzindua chuo anuwai cha Ngeria TTI katika kaunti ya Uasin Gishu, kiongozi wa taifa alisema vijana wengi wanafaidika kutoka kwa matumizi mazuri ya mitandao ya kijamii na utandawazi, huku akiwasuta wale wanaotumiwa vibaya kueneza chuki na propaganda dhidi ya viongozi wa nchi.


Ruto alisema kwamba kuna baadhi ya wanasiasa ambao sasa wanawalipa vijana wenye ujuzi wa kutumia akili mnemba (AI) kutengeneza picha za viongozi wakiwa kwenye majeneza na makaburi.


“Mimi nawauliza vijana wale wengine, wasipotoshwe na wanasiasa wa kuwalipa pesa kidogo eti waweke picha za viongozi eti kwenye makaburi. Mimi nataka niwaambie hawa vijana, leo mtaweka viongozi kwenye kaburi kesho mtaweka wazazi wenu kwenye kaburi na keshokutwa mtaweka wenzenu, marafiki zenu na siku nyingine ni nyinyi mtaanza mambo ya mauaji,” Ruto alisema.


 Rais pia alisema kwamba wale wanaowatia moyo vijana kuendelea na hulka hiyo ya kuwakoshea heshima mitandaoni viongozi wao kukoma mara moja kwani ni vizuri kuwafunza vijana tabia njema.


“Ningependa kuwaambia wale wanaowaweka viongozi kwenye majeneza, kwamba ni lazima tuwaambie vijana kwamba tabia njema hulipa. Badala ya kutumia mtandao kuweka picha za viongozi kwenye majeneza, tumia mtandao kutengeneza pesa na kupata ajira kwenye nyinyi na kuboresha maisha yenu,” rais aliongeza.


Mkuu wa taifa alisema kwamba kwa sasa vijana wa Kenya zaidi ya 120,000 wanatengeneza pesa kutoka kwa mitandao ya kijamii kutokana na matumizi mazuri ya mitandao hiyo.


“Ninajivunia sana vijana ambao nimeona kwenye hii TVET, wale vijana ambao wanatengeneza pesa, wanaweka pesa kwa mfuko, pesa ya madola kwa sababu ya kutumia intaneti, waweze kupanga mambo yao ya ajira, na kuweza kufanya kazi le ya digital jobs. Na tuko na vijana elfu 120 Kenya ambao tayari wanafanya kazi katika Digital jobs na kuweka pesa zao kwa mfuko,” Ruto aliongeza.


Kiongozi wa taifa atakamilisha ziara yake ya siku tatu Jumamosi katika ukanda wa Bonde la Ufa Kaskazini ya siku tatu ambayo iling’oa nanga Alhamisi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved