logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Kama Kenya Ni Mbaya Si Upotee!” MP Elachi Kwa Wanaolalamikia uongozi wa Ruto

"Kama Kenya ni mbaya unafanya nini hapa mahali pabaya? Na kama hupotei basi ujue hii ni nchi yako na hakuna mahali utaenda,” Elachi alifoka.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari13 January 2025 - 16:27

Muhtasari




    MBUNGE wa Dagoretti Kaskazini, Beatrice Elachi amewataka wanaodai kwamba Kenya inaelekea katika mkondo mbaya chini ya uongozi wa rais William Ruto kuondoka nchini.


    Mbunge huyo ambaye alikuwa akizungumza Jumapili katika ibada ya kanisa kwenye Eneobunge hilo, ibada ambayo ilihudhuriwa na rais alisema kwamba amekuwa katika uwanja wa ndege juzi na aliona jinsi watu wengi wana uchu wa kutoka nje wakitembelea Kenya.


    Elachi alisema kwamba aliona jinsi watalii wengi kutoka nje wamefurika uwanja wa ndege wakiwa na nia ya kutalii Kenya na wakati uo huo kuna Wakenya wengi kwenye mitandao ya kijamii wanateta kwamba Kenya ni mbaya.


    Elachi aliwataka wale wanaoteta kwamba Kenya ni mbaya kupoteza kutoka nchini kuliko kuchochea wengine kuamini katika dhana hiyo.


    “Ni lazima tutengeneze uwanja wa ndege mheshimiwa rais. Nimekuwa huko juzi wageni wakitoka USA madaktari. Watu walikuwa wamejaa nje, walikuwa wanaondoka na wengine wanaingia…”


    “Wale wageni wanaingia Kenya wanasema Kenya ni nchi nzuri, na Mkenya ako hapa anasema eti Kenya ni mbaya. Kama Kenya ni mbaya si upotee! Kama Kenya ni mbaya unafanya nini hapa mahali pabaya? Na kama hupotei basi ujue hii ni nchi yako na hakuna mahali utaenda,” Elachi alifoka.


    Mbunge huyo alisema kwamba Mkenya akienda nchi yoyote kwa sasa watamkataa kwa vile watahisi kwamba anaenda kuwaharibia nchi kwa vile nyumbani hawamheshimu rais wao.


    “Ukienda Dar es Salaam watakuangalia wanasema hawa Wakenya wanatusi mpaka viongozi wao, hawa wanakuja kutuharibia nchi yetu. Sasa utaenda wapi?” Elachi aliuliza.


    Alitoa wito kwa Wakenya kumheshimu rais Ruto, akisema kwamba kwa kufanya hivyo, watabarikiwa.


    “Tulinde nchi yetu, tuheshimu mheshimiwa rais. Na tukimheshimu tutabarikiwa ndio shilingi yetu iimarike [dhidi ya sarafu za kigeni],” mbunge huyo wa Dagoretti North alirai.


    Wakati uo huo, kiongozi wa taifa alisema kwamba anajihisi mwenye fahari kubwa kuwa rais wa Kenya, akisisitiza kwamba ana wajibu mkuu kutoka kwa Mungu kubadilisha hii nchi.


    Rais alitoa rai kwa Wakenya kuunga serikali mkono katika jitihada zake za kuhakikisha uchumi wa nchi unaimarika ili kurahisisha maisha ya Mkenya wa kawaida.


     



    RADIO JAMBO FREQUENCIES

    Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


    logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved