logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ruto: Sijali kuitwa Kasongo au Zakayo

“Unajua mimi ni mwerevu kuliko baadhi ya watu waliojitokeza kuniita Kasongo, na Zakayo, hilo sina tatizo ilimradi maendeleo yapo.

image
na Tony Mballa

Habari24 January 2025 - 17:51

Muhtasari


  • Wimbo maarufu "Kasongo" uliimbwa kwa mara ya kwanza mnamo 1967 na Super Mazembe, bendi ya soukous ya Kenya kutoka Zaire (sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo).
  •  Wimbo huo "Kasongo," ulioandikwa na mwimbaji mashuhuri Alley Katele, ambaye pia alianza kuimba wimbo huo, unamshirikisha mwanamke akimsihi mume wake aliyeachana naye arejee nyumbani.




Rais William Ruto amesema yuko sawa na jina lake la utani, "Kasongo," mradi tu nchi ifanye maendeleo.

Akizungumza siku ya Ijumaa katika ziara yake ya Kanda ya Magharibi, Rais Ruto alisema kuwa Wakenya wanamtaja kama 'Kasongo' kwa sababu ni mtu mwenye busara.

“Unajua mimi ni mwerevu kuliko baadhi ya watu waliojitokeza kuniita Kasongo, na Zakayo, hilo sina tatizo ilimradi maendeleo yapo.

Wimbo maarufu "Kasongo" uliimbwa kwa mara ya kwanza mnamo 1967 na Super Mazembe, bendi ya soukous ya Kenya kutoka Zaire (sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo).

Wimbo huo "Kasongo," ulioandikwa na mwimbaji mashuhuri Alley Katele, ambaye pia alianza kuimba wimbo huo, unamshirikisha mwanamke akimsihi mume wake aliyeachana naye arejee nyumbani.

Super Orchestra Mazembe ilikuwa bendi maarufu inayopiga muziki wa Soukous ambao  walihama kutoka Zaire hadi Nairobi mwaka wa 1974 wakibadilisha jina lao kutoka Super Vox.

Jina lao linatafsiriwa kwa "wasogezi wa dunia kubwa. ‘Baadhi ya nyimbo maarufu za kundi hilo ni pamoja na Shauri Yako, Bwana Nipe Pesa na Samba. Kasongo alitungwa wakati wana bendi walipoenda kumtembelea rafiki yao Kasongo huko Eastleigh, Nairobi. 

Walipofika nyumbani kwake, walikutana na mke wa Kasongo, na wakamuuliza kama alikuwa nyumbani.

Mke wa Kasongo aliwakaribisha na kuwaambia kwamba alikuwa hajamwona Kasongo kwa siku nyingi. Wakati huo, hakukuwa na mtandao na ilikuwa nadra kupata mtu anayemiliki simu.

Waliamua kumtumia ujumbe kwa njia ya muziki, wakitumaini kwamba ungemfikia. Wanachama wa Super Mazembe walianza kumtengenezea Kasongo wimbo sebuleni kwake, wakimwambia arudi nyumbani kwa sababu mkewe ana wasiwasi na anamtafuta lakini hampati.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved