logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nick Mwendwa atiwa mbaroni tena baada ya faili ya kesi yake kufungwa

Ripoti hizo zilithibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa FKF Barry Otieno mnamo Ijumaa.

image
na Radio Jambo

Habari26 November 2021 - 11:08

Muhtasari


  • Ripoti hizo zilithibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa FKF Barry Otieno mnamo Ijumaa
  •  Mwendwa anazuiliwa katika Makao Makuu ya DCI kando ya Barabara ya Kiambu
  • Mnamo Alhamisi, upande wa mashtaka uliambia mahakama kwamba ungependa kuifunga kesi hiyo kwa sasa

Rais wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF) Nick Mwendwa amekamatwa tena.

Ripoti hizo zilithibitishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa FKF Barry Otieno mnamo Ijumaa.

 Mwendwa anazuiliwa katika Makao Makuu ya DCI kando ya Barabara ya Kiambu.

Mnamo Alhamisi, upande wa mashtaka uliambia mahakama kwamba ungependa kuifunga kesi hiyo kwa sasa.

DPP alikuwa amepatiwa siku saba kupendekeza mashtaka dhidi ya Mwendwa lakini amechagua kufunga faili yake.

"Tunataka kufunga faili yetu huku timu yetu ikiendelea na uchunguzi wa kesi hiyo kwa kasi yetu kabla ya kupendekeza mashtaka dhidi yake," alisema DPP.

Hakimu mfawidhi wa mahakama ya Milimani Wandia Nyamu aliruhusu ombi la DPP na kuamuru kesi hiyo kufungwa.

Siku ya Alhamisi DPP na DCI walitarajiwa kufahamisha mahakama iwapo walikuwa wamekamilisha uchunguzi dhidi ya Mwendwa na kupendekeza mashtaka yafaayo.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved