logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kalonzo njia panda KANU ikiashiria kujiunga na Azimio

Gideon Moi ameashiria huenda KANU ikajiunga na Azximio la Umoja hivi karibuni.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri09 March 2022 - 03:53

Muhtasari


• Gideon Moi wa KANU ameashiria utayarifu wao kujiunga na muungano wa Azimio la Umoja na kuweka mustakabali wa OKA katika njia panda.

Kiongozi wa chama cha KANU Gideon Moi ambaye pia ni mmoja wa vinara wa muungano wa kisiasa wa OKA ameashiria kwamba huenda chama hicho kikatoa tangazo hivi karibuni la kujiunga na muungano wa Azimio la Umoja unaoongozwa na kinara wa ODM Raila Odinga na hivyo kuweka mustakabali wa OKA katika njia panda.

Akizungumza katika hafla ya kuzindua kampeni za mbunge wa Samburu Magharibi Naisura Lesuuda, Moi aliashiria kwamba katika mkutano wa wanachama unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni, huenda wakatangaza rasmi kuwa miongoni mwa Azimio la Umoja.

“Kwa ndugu zangu, kwa sasa unajua harakati hii ambayo sisi sote tunaelekea. Sisi kama wanachama wa KANU tuko na mrengo na nyinyi kwa hii Azimio, sisi sote tuko Pamoja. Hivi karibuni kwa maneno nyinyi wote mtasikia,” alisema Moi katika mkutano huo ambao pia ulihudhuriwa na kiongozi wa ODM Raila Odinga.

Moi pia alisisitiza kuwa iwapo wataungana na Azimio basi wawe kitu kimoja.

“Lakini tafadhali tafadhali, tukae sisi sote kitu kimoja.”

Matamshi haya ya Moi yanamweka katika njia panda kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka ambaye pia analenga kuwania urais kupitia mrengo wa OKA, huku wengi wakihoji kwamba huenda hatimaye mrengo huo ukasambaratika na vinara waliosalia kujiunga na marengo mingine kama Kenya Kwanza na Azimio la Umoja.

Mrengo huo wa OKA ulianza kuyumba mapema mwaka huu pale ambapo kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi na mwenzake wa FORD-K Moses Wetengula walipogura na kujiunga na naibu rais William Ruto ambapo walianzisha muungano wa Kenya Kwanza.

Je, unahisi ndio mwisho wa reli kwa muungano wa OKA? Mustakabali wa kisiasa wa Kalonzo utakuwa upi baada ya Moi kuashiria huenda KANU  wakajiunga na Azimio?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved