logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Raila Odinga aagizwa kufika mbele ya NCIC kufuatia matamshi yake "madoadoa"

NCIC imetaja matamshi hayo ambayo Raila alitoa Jumatano kuwa ya chuki.

image
na Radio Jambo

Burudani11 March 2022 - 10:41

Muhtasari


•NCIC inamtaka Raila aeleze matumizi yake ya hivi majuzi ya neno 'madoadoa' katika mkutano wa Azimio la Umoja wa hivi majuzi katika kaunti ya Wajir.

Tume ya Tume ya Uwiano na Utangamano wa Kitaifa (NCIC) imeuagiza kinara wa ODM kufika mbele yake kufuatia matamshi "madoadoa" aliyotoa katika kaunti ya Wajir.

Kupitia taarifa iliyotolewa Ijumaa, NCIC imetaja matamshi hayo ambayo Raila alitoa Jumatano kuwa ya chuki.

"Tume ingependa kuwahakikishia Wakenya kuhusu kujitolea kwake kuzuia aina yoyote ya matamshi ya chuki ili kuhakikisha Kenya inasalia kuwa taifa tulivu, lenye ustawi na mshikamano na kutimiza ahadi yetu ya 'uchaguzi bila noma'," Taarifa ya NCIC ilisoma.

NCIC inamtaka Raila aeleze matumizi yake ya hivi majuzi ya neno 'madoadoa' katika mkutano wa Azimio la Umoja wa hivi majuzi katika kaunti ya Wajir.

Raila aliwaomba wakazi wa Wajir kuunga mkono wagombea wa vuguvugu la Azimio La Umoja katika uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti.

Raila alisema kuwa vuguvugu hilo lina vyama vingi ambavyo vimeungana ili kuunganisha nchi, hivyo basi haja ya kulipigia kura.

Mengine yanafuata...


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved