logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mahakama ya upeo imedumisha ushindi wa Ruto kama rais wa 5 wa Kenya

Mahakama iliidhinisha ushindi wa William Ruto kama rais mteule wa taifa la Kenya.

image
na Radio Jambo

Habari05 September 2022 - 09:03

Muhtasari


• Majaji wa mahakama ya upeo ni Jaji mkuu Martha Koome, naibu jaji mkuu Philomena Mwilu, Smokin Wanjala, Njoki Ndung'u, Isaac Lenaola, William Ouko na Mohamed Ibrahim.

Rais wa tano wa Kenya

Ni rasmi sasa kwamba William Ruto  atakuwa rais wa tano wa Kenya.

Hii ni baada ya Jopo la majaji saba wa mahakama ya upeo likiongozwa na jaji mkuu Martha Koome kuidhinisha ushindi wa rais mteule William Ruto.

Jopo hilo likisoma uamuzi wake lilisema kwamba kesi iliyowasilishwa katika mahakama hiyo na muungano wa Azimio la Umoja pamoja na mashirika mengine haikudhihirisha wazi malalamisho yao haikuwa na uzito unaoweza kufanya ushindi wa Ruto kubatilishwa.

Kando na jaji mkuu Martha Koome, majaji wengine walikuwa ni pamoja na naibu jaji mkuu Philomena Mwilu, Smokin Wanjala, Njoki Ndung'u, Isaac Lenaola, William Ouko na Mohamed Ibrahim.

Mahakama hiyo ilitupilia mbali madai yote yalioibuliwa na waliopinga ushindi wa Ruto na ikiwemo kuafikia kigezo cha sheria kuwa mshindi wa urais anafaa kufikisha asilimia 50+1.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved