logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Basi lililojaa abiria latumbukia kwenye mto Kisii

Idadi kamili ya watu waliokuwa kwenye basi hilo haijajulikana.

image
na

Habari26 November 2022 - 07:43

Muhtasari


  • Abiria waliojeruhiwa walipelekwa katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Kisii, kilomita saba kutoka eneo la ajali

Basi la abiria linalomilikiwa na kampuni ya huduma ya Guardian Bus limetumbukia kwenye mto Kisii.

Ripoti zilizofikia Radiojambo zinaonyesha kuwa mkasa huo ulitokea Nyamarambe kaunti ya Kisii.

Idadi kamili ya watu waliokuwa kwenye basi hilo haijajulikana.

Ripoti zilidai kuwa abiria kadhaa walipata majeraha mabaya wakati wa ajali hiyo.

Abiria waliojeruhiwa walipelekwa katika Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Kisii, kilomita saba kutoka eneo la ajali.

Shughuli za uokoaji wa dharura zinaendelea kwa sasa, huku wakazi na watoa huduma wakiwasaidia majeruhi.

Chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana hadi wakati wa kuchapishwa kwa habari hii.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved