logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mbunge afariki baada ya kugongwa na bodaboda South B, Nairobi

Kulow atazikwa jioni ya leo Jumatano katika masihara ya Lang'ata.

image
na Radio Jambo

Habari29 March 2023 - 04:11

Muhtasari


• Mbunge huyo aligongwa na pikipiki na kupata majeraha ya kichwa.

• Mbunge huyo atazikwa mwendo wa saa kumi jioni ya leo Jumatano katika makaburi ya waislamu eneo la Lang’ata jijini Nairobi.

Kulow Maalim, Banisa MP

Mbunge wa Banissa, Kulow Hassan Maalim amefariki dunia baada ya kugongwa na bodaboda siku ya Jumapili katika mtaa wa South B jijini Nairobi.

Kulingana na ripoti kutoka kwa familia yake, Mbunge huyo kutoka kaunti ya Garissa alifariki mapema alfajiri ya Jumatano katika kituo kimoja cha afya alikokuwa akipata matibabu.

Mbunge huyo aligongwa na pikipiki na kupata majeraha ya kichwa.

Mbunge huyo atazikwa mwendo wa saa kumi jioni ya leo Jumatano katika makaburi ya waislamu eneo la Lang’ata jijini Nairobi.

Marehemu mbunge amewakilisha eneo bunge la Banissa katika Bunge la Agosti tangu 2017. Pia aliwahi kuwa mwanachama wa Kamati ya Idara ya Uchukuzi, Kazi za Umma na Makazi.

Wenzake, wakiongozwa na mbunge wa Eldas Adan Keynan wamemwomboleza kama kiongozi mashuhuri na mtumishi wa umma aliyejitolea.

"Kulow alikuwa kielelezo cha kiongozi mashuhuri, mtumishi wa umma aliyejitolea na mtu anayependeza katika jamii ambaye alitekeleza majukumu yake ya uongozi kwa heshima na ustadi mkubwa," Keynan alisema.Mbunge wa Mandera Magharibi Adan Haji Yussuf Adan Haji alituma salamu za rambirambi kwa wananchi wa Banissa na familia ya marehemu mwenzake.

"Maalim alikuwa kiongozi mkuu na Muislamu aliyejitolea ambaye amekuwa na nafasi muhimu katika jamii yetu," alisema.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved