logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wikendi ndefu! Serikali yatangaza Jumatatu, Juni 17 kuwa Sikukuu ya Umma

Waziri wa Usalama wa Ndani Kithure Kindiki ametangaza Jumatatu, Juni 17 kuwa sikukuu ya umma.

image
na SAMUEL MAINA

Habari14 June 2024 - 05:35

Muhtasari


  • •Waziri wa Usalama wa Ndani Kithure Kindiki ametangaza Jumatatu, Juni 17 kuwa sikukuu ya umma.
Waziri wa usalama wa ndani Kithure Kindiki

Jiandae kwa wikendi ndefu!

Serikali ya Kenya, kupitia waziri wa Usalama wa Ndani Kithure Kindiki imetangaza  siku ya Jumatatu, Juni 17 kuwa sikukuu ya umma.

Sikukuu hiyo imetangazwa kwenye gazeti rasmi ya serikali. Siku hiyo imetengwa kuadhimisha Eid-Al-Adha.

Sherehe ya Eid-ul-Adha ni kukumbuka kujitolea kwa Nabii Ibrahim kwa Mwenyezi Mungu na utayari wake wa kumchinja mwanawe, Ismail.

Sikukuu ya Sadaka ni mojawapo ya sikukuu mbili muhimu za Uislamu.

Ni muhimu hasa kwa sababu ni alama ya mwisho wa Hija ya kila mwaka au Hija ya Makka, inayoadhimishwa katika mwezi wa mwisho wa kalenda ya Kiislamu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved