Waandamanaji hatimaye waingia ndani ya Bunge

Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Kenya kwa waandamanaji kuvunja vizuizi na kuingia ndani ya Bunge licha ya ulinzi mkali.

Muhtasari

• Waandamanaji hao pia walichoma idadi ya magari ya Polisi huku hali ya wasiwasi ikiongezeka nje ya bunge la nchi hiyo.

Waandamanaji wa Muswada wa Kupinga Mswada wa Fedha katika mamia yao Jumanne mchana waliingia ndani ya Bunge.

Waandamanaji hao waliingia ndani ya Bunge saa chache baada ya polisi kuwapiga risasi waandamanaji kadhaa nje ya Majengo ya Bunge.

Waandamanaji hao pia walichoma idadi ya magari ya Polisi huku hali ya wasiwasi ikiongezeka nje ya bunge la nchi hiyo.

Muda kidogo, Wabunge walikuwa wamepiga kura kuidhinisha Mswada wa Fedha wa 2024 ambao ulibishaniwa unaweka wimbi la ushuru.

Hii ni mara ya kwanza katika historia ya Kenya kwa waandamanaji kuvunja vizuizi na kuingia ndani ya Bunge licha ya ulinzi mkali.

Hapo awali, polisi walikuwa wamefaulu kuwazuia waandamanaji kuingia Bungeni na kila mara walizingira ulinzi.