Sikuamini mtoto wa Sugoi siku moja angekuwa rais wa Kenya- Rais William Ruto

William Ruto aliona mustakabali wake kama Rais wa Kenya wakati wa sherehe ya uamsho iliyofanyika Marekani mwaka wa 2006.

Muhtasari
  • Wakati wa uponyaji ya Kasisi Benny Hinn Jumapili, Ruto alisema alikuwa na mkewe Rachel wakati wa ufichuzi huo.
Atangaza kufuta madeni yote ya viwanda vya sukari
WILLIAM RUTO// Atangaza kufuta madeni yote ya viwanda vya sukari
Image: FACEBOOK

William Ruto aliona mustakabali wake kama Rais wa Kenya wakati wa sherehe ya uamsho iliyofanyika Marekani mwaka wa 2006.

Wakati wa uponyaji ya Kasisi Benny Hinn Jumapili, Ruto alisema alikuwa na mkewe Rachel wakati wa ufichuzi huo.

"Mara ya kwanza nilipopata ufunuo kwamba nitakuwa rais nchini Kenya ilikuwa mwaka wa 2006 wakati wa sherehe za uamsho wa Asuza 100 nchini Marekani na nilikuwa huko na mke wangu na Mchungaji Askofu Adoyo na wengine wengi," Rais alieleza.

Rais alisema kuwa wakati huo, hakuamini.

"Sikuamini kuwa mtoto wa Sugoi siku moja angekuwa rais wa Kenya".

Ruto alisema kwamba alikuwa na hakika kwamba Bwana angependelea Kenya kwa ufunuo mwingine na kwamba Kenya ingekuwa taifa kubwa, sio tu barani Afrika bali ulimwenguni kote.

Pia alitaja kuwa mnamo 2023, kulikuwa na ukame mkubwa nchini Kenya na baada ya maombi katika uwanja wa Nyayo, nchi ilipata mvua bora zaidi katika miaka 10 iliyopita.

""Nimetoka kwenye mkutano na balozi wa Marekani. Alikuja kuniambia kuwa Rais wa Marekani amemwalika Rais wa Kenya kwa ziara ya kiserikali, ya aina yake. Katika miaka 20, hakuna Rais wa Afrika ambaye amekuwa na ziara ya kiserikali nchini Marekani,” Ruto aliongeza. 

Vita vya uamsho vilifanyika katika Uwanja wa Kitaifa wa Nyayo jijini Nairobi ambapo mwinjilisti Benny Hinn alihudumia umati uliokuwepo.

Rais Ruto alihudhuria pamoja na Mkewe, Rachel Ruto, na binti yao Charlene Ruto.