Tazama vitu maalum ambavyo Zari alimuomba Mungu amjalie mume wake Shakib Lutaaya

Miongoni mwa mambo ambayo Zari aliombea ni pamoja na mumewe kuto'cheat, kutorukaruka nje ya ndoa, na kutoponda raha.

Muhtasari

•Zari alitaja vitu ambavyyo angetaka Shakib apewe ikiwa ni pamoja na gari la kifahari, jumba kubwa la kifahari, mabinti wawili na uaminifu katika ndoa.

maalum ambavyo Zari alimuomba Mungu amjalie mumewe
Vitu maalum ambavyo Zari alimuomba Mungu amjalie mumewe
Image: ROSA MUMANYI

Mwanasholaiti maarufu wa Uganda Zari Hassan na mumewe Shakib Cham Lutaaya hivi majuzi walifanya maombi ya pamoja ambapo walimwomba Mungu awape vitu kadhaa maalum.

Katika video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Zari alisikika akitaja vitu ambavyo wangetaka kujaliwa navyo huku mumewe akisema ‘Amina’ baada ya kila kitu kilichotajwa.

Mama huyo wa watoto watano alianza kwa kutaja vitu ambavyyo angetaka Shakib apewe ikiwa ni pamoja na gari la kifahari, jumba kubwa la kifahari, mabinti wawili na uaminifu katika ndoa.