logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rais wa Haiti auawa katika shambulizi kwenye makazi yake

Mke wa Rais aliripotiwa pia kujeruhiwa katika shambulio hilo.

image
na Radio Jambo

Habari07 July 2021 - 11:02

Muhtasari


  • Rais wa Haiti auawa katika shambulizi kwenye makazi yake
  • Mke wa Rais aliripotiwa pia kujeruhiwa katika shambulio hilo

Rais wa Haiti Jovenel Moise ameuawa katika shambulio dhidi ya makazi yake mjini Port-au-Prince - amesema kaimu Waziri mkuu Claude Joseph

Bwana Joseph alisema makazi ya rais huko Port-au-Prince yalishambuliwa na watu wasiojulikana waliojihami kwa silaha saa 01:00 saa za eneo hilo (05:00 GMT).

Mke wa Rais aliripotiwa pia kujeruhiwa katika shambulio hilo.

Bwana Joseph alisema kuwa "hatua zote zilichukuliwa ili kuhakikisha kuendelea kwa serikali".

Jovenel Moïse, 53, alikuwa madarakani tangu Februari 2017, baada ya mtangulizi wake, Michel Martelly kung'atuka mamlakani.

Wakati wa Bw Moïse ofisini ulikuwa mgumu wakati alipokabiliwa na tuhuma za ufisadi na alikabiliwa na mawimbi ya maandamano ya mara kwa mara ya kupinga serikali

Mwaka wa 2019 wakati wa mojawapo ya maandamano kama hayo rais huyo alisema 'Hatondoka nchini kwasababu ya shinikizo kutoka kwa magenge yaliyojihami na walanguzi wa dawa za kulevya'

Kulikuwa na maandamano yaliyoenea katika mji mkuu na miji mingine mapema mwaka huu, kwani watu walimtaka ajiuzulu.

Upinzani nchini humo ulisema kwamba kipindi cha miaka mitano cha Bw Moïse kilipaswa kumalizika tarehe 7 Februari 2021, miaka mitano hadi siku hiyo tangu Bw Martelly aondoke madarakani.

Bwana Moïse, hata hivyo, alisisitiza alikuwa na mwaka mmoja zaidi wa kutumikia kwani hakuingia madarakani hadi 7 Februari 2017.

Kucheleweshwa kwa mwaka mzima kulisababishwa na madai ya udanganyifu katika uchaguzi ambao mwishowe ulisababisha matokeo ya uchaguzi wa 2015 kufutiliwa mbali na kura mpya kufanywa ambapo Bw Moïse alitangazwa mshindi .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved