logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii nyota wa Hip hop nchini Rwanda afariki ghafla

RCS bado haijatoa maelezo kuhusu kifo cha nyota huyo wa muziki.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri02 September 2021 - 10:45

Muhtasari


  • Msanii nyota muziki wa Hip hop wa Rwanda Joshua Tuyishime al maarufu Jay Polly, amefariki ghafla katika hospitali jijini Kigali, kaka yake ameithibitishia BBC

Msanii nyota muziki wa Hip hop wa Rwanda Joshua Tuyishime al maarufu Jay Polly, amefariki ghafla katika hospitali jijini Kigali, kaka yake ameithibitishia BBC.

Vyombo vya habari nchini humo zinasema kuwa Joshua Tuyishime alikimbizwa hospitalini kutoka gereza kuu laKigali baada ya kupatwa na ugonjwa usiojulikana Jumatano usiku.

Jay Polly mwenye umri wa miaka 33 alikamatwa mwezi Aprili kwa makossa ya matumizi ya dawa za kulevya, na kesi yake ilikuwa inaendelea.

Kaka yake Maurice Uwera amesema kuwa mamlaka ya huduma za magereza nchini Rwanda , “imeniambia”kuhusu kifo chake, lakini hakutoa maelezo zaidi.

RCS bado haijatoa maelezo kuhusu kifo cha nyota huyo wa muziki.

Mashabiki wengi wa muziki nchini Rwanda ambao walimfahamu Jay Polly kwa zaidi ya muongowamuziki wake wamekuwa wakitoa rambi rambi zao kupitia mitandao ya kijamii.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved