logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Guinea yafukuzwa kutoka Jumuiya ya ECOWAS kufuatia mapinduzi ya kijeshi

Viongozi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi ECOWAS wameiondoa Guinea kutoka jumuiya hio kufuatia mapinduzi ya kijeshi ya Jumapili ambayo yalimwondoa Rais Alpha Conde madarakani

image
na Radio Jambo

Burudani09 September 2021 - 05:55

Viongozi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Mataifa ya Afrika Magharibi ECOWAS wameiondoa Guinea kutoka jumuiya hio kufuatia mapinduzi ya kijeshi ya Jumapili ambayo yalimwondoa Rais Alpha Conde madarakani .

Uamuzi huo ulichukuliwa kufuatia mkutano uliofanywa kwa njia ya mtandao Jumatano. Kulingana na Reuters, uamuzi huo ulitangazwa na Waziri wa Mambo ya nje wa Burkina Faso, Alpha Barry.

Rais Nana Akufo-Addo wa Ghana ambaye pia ni mwenyekiti wa ECOWAS alisema kuwa mapinduzi ya kijeshi yalikiuka makubaliano ya jumuiya hiyo kuhusu utawala bora.

Umoja wa Afrika na ECOWAS wamelaani mapinduzi hayo ya kijeshi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved