logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ufaransa inachunguza ubakaji wa askari katika ikulu ya Élysée

Yeye na mtuhumiwa wote wamehamishwa kwa majukumu mengine, ikulu ilisema.

image
na Radio Jambo

Habari12 November 2021 - 20:16

Muhtasari


  • Rais Emmanuel Macron alikuwa amehudhuria hafla hiyo, iliyofanyika kwa wafanyikazi wanaoondoka
  • Mtuhumiwa - pia mwanajeshi - amehojiwa, lakini bado hajafunguliwa mashtaka rasmi, ripoti zinasema

Waendesha mashtaka wa Ufaransa wamefungua uchunguzi kuhusu madai ya ubakaji katika ikulu ya rais mjini Paris.

Vyombo vya habari nchini humo vinaripoti kwamba mwanajeshi wa kike amesema alinajisiwa baada ya tafrija ya vinywaji katika jumba la Élysée mwezi Julai.

Rais Emmanuel Macron alikuwa amehudhuria hafla hiyo, iliyofanyika kwa wafanyikazi wanaoondoka.

Mtuhumiwa - pia mwanajeshi - amehojiwa, lakini bado hajafunguliwa mashtaka rasmi, ripoti zinasema.

Gazeti la Libération liliripoti kwanza mashtaka hayo siku ya Ijumaa.

Wote wawili wanaodaiwa kuwa mwathiriwa na mshambulizi waliripotiwa kufanya kazi katika ofisi ya wafanyakazi wa ulinzi mkali katika jengo hilo, na Libération ilisema wanafahamiana.

Afisa wa rais aliliambia shirika la habari la AFP kwamba "mara tu mamlaka zilipofahamu madai haya, hatua zilichukuliwa mara moja" kumsaidia mwathiriwa huyo.

Yeye na mtuhumiwa wote wamehamishwa kwa majukumu mengine, ikulu ilisema.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved