logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wafungwa 38 wafariki, 69 wajeruhiwa katika mkasa wa moto gerezani Burundi

Kumi na wawili kati ya waliofariki walisakamwa na moshi huku 26 waliosalia wakipata majeraha ya moto,

image
na Radio Jambo

Burudani08 December 2021 - 06:47

Muhtasari


•Kumi na wawili kati ya waliofariki walisakamwa na moshi huku 26 waliosalia wakipata majeraha ya moto,

Moto mkubwa

Takriban wafungwa 38 wamefariki dunia na wengine 69 kujeruhiwa katika moto ulioteketeza gereza kuu la mji mkuu wa kisiasi wa Burundi Gitega mapema Jumanne.

Haijabainika ni nini kilisababisha moto huo.

Kumi na wawili kati ya waliofariki walisakamwa na moshi huku 26 waliosalia wakipata majeraha ya moto, kulingana na makamu wa rais wa Burundi, Prosper Bazombanza, ambaye alitembelea kituo hicho na hospitali ambapo wengi wa majeruhi wanatibiwa.

Aliwaambia waandishi wa habari kuwa majeruhi 34 waliopata majeraha ya moto ya wastani na zaidi wamepelekwa hospitali huku wengine wakipatiwa matibabu katika eneo la gereza.

"Wafanyikazi wa afya wametupa hakikisho kwamba watapona", alisema.

Afisa huyo pia alitangaza bili yao ya matibabu italipwa kikamilifu na serikali.

Hali mbaya ya usalama ilifanya iwe rahisi kwa moto huo kuenea haraka katika gereza ambalo awali lilikusudiwa watu 400 lakini sasa lilikuwa na wafungwa zaidi ya 1500.

Kiwango kamili cha uharibifu kilikuwa bado hakijajulikana.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved