logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Corona: Rais wa Msumbiji na mke wake wamejitenga

Kumekuwa na ongezeko la virusi vya corona katika siku za hivi karibuni nchini Msumbiji.

image
na Radio Jambo

Habari04 January 2022 - 09:51

Muhtasari


  • Taarifa hiyo ilisema waliamua kufanya vipimo baada ya "shughuli walizokuwa nazo siku chache zilizopita 
  • Kumekuwa na ongezeko la virusi vya corona katika siku za hivi karibuni nchini Msumbiji

Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi na mke wake Isaura Nyusi wamekutwa na virusi vya corona na wamejitenga kwa sasa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi ya rais Bw. Nyusi na mke wake wameamua kujitenga kwa kuzingatia muongozo wa afya baada ya kupatikana na virusi , ijapokuwa hawakuonesha dalili zozote.

Taarifa hiyo ilisema waliamua kufanya vipimo baada ya "shughuli walizokuwa nazo siku chache zilizopita ".

Kumekuwa na ongezeko la virusi vya corona katika siku za hivi karibuni nchini Msumbiji.

Nchi hiyo imethibitisha kuwa na watu 193,000 wanaougua Covid-19, huku vifo 2,031 vikirekodiwa.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved