Mlipuko mkubwa watokea mjini Mogadishu, Somalia

Hadi wakati wa kuchapisha taarifa hii ilikuwa haijabainika kilichosababisha mlipuko huo

Muhtasari

• Kulingana na ripoti za Reuters baadhi ya miili ilikuwa ilionekana karibu na eneo la mlipuko.

• Mhudumu wa afya alionekana akimhudumia angalau mtu mmoja aliyejeruhiwa.

Eneo la mlipuko katika wilaya ya Hamarweyne ya Mogadishu, Somalia, Januari 12, 2022. Picha: REUTERS/Feisal Omar
Eneo la mlipuko katika wilaya ya Hamarweyne ya Mogadishu, Somalia, Januari 12, 2022. Picha: REUTERS/Feisal Omar

Mlipuko mkubwa ulitokea katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu siku ya Jumatano kwenye barabara inayoelekea uwanja wa ndege. 

Kulingana na ripoti za Reuters baadhi ya miili ilikuwa ilionekana karibu na eneo la mlipuko. Mlipuko huo uliharibu magari manne na tuk tuk mbili.

Hadi wakati wa kuchapisha taarifa hii ilikuwa haijabainika kilichosababisha mlipuko huo. 

Mhudumu wa afya alionekana akimhudumia angalau mtu mmoja aliyejeruhiwa.