logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanzania yakanusha madai ya utekaji nyara katika mbuga ya Serengeti

Watu kadhaa wanadaiwa kutoweka baada ya kukamatwa na maaskari wa mbuga hiyo.

image
na Radio Jambo

Habari03 May 2022 - 12:09

Muhtasari


•Watu kadhaa wanadaiwa kutoweka miezi kadhaa baada ya kukamatwa katika hali isiojulikana na wale wanaodaiwa kuwa maaskari wa mbuga hiyo.

Shirika la mbuga za kitaifa za wanyapori nchini Tanzania limekana ripoti kwamba maafisa wake waliwanyanyasa na kuwateka wakaazi katika mbuga ya wanyamapori ya Serengeti.

Hatua hiyo inajiri kufuatia madai kwamba baadhi ya watu wametoweka miezi kadhaa baada ya kukamatwa katika hali isiojulikana na wale wanaodaiwa kuwa maaskari wa mbuga hiyo.

Katika taarifa , Shirika la kitaifa la mbuga za wanyamapori nchini Tanzania Tanapa , limesema kwamba halijapokea ripoti zozote zilizo rasmi kuhusu unyanyasaji huo uliotekelezwa na askari wa Wanyama pori wala ripoti kuhusu raia waliodaiwa kutoweka.

Iliwashauri wale wanaomiliki mitandao ya kijamii kuthibitisha habari wanazopokea ili kutosababisha hali ya wasiwasikuhusu masuala yanayohusu maisha ya binadamu.

Tanapa imesema kwamba itaendelea kuchukua jukumu lake la kuhifadhi mbuga za Wanyama pori za taifa hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved