Tumbili aiba ushahidi muhimu kwenye kesi ya mauaji mahakamani

Muhtasari

•Inaripotiwa ushahidi ulioibiwa na tumbili huyo ni pamoja na kisu kinachoaminika kutumika katika mauaji hayo.

Image: BBC

Kesi ya mauaji ya mwaka 2016 nchini India imeahirishwa baada ya polisi kusema ushahidi uliokusanywa uliibiwa na tumbili.

Gazeti la The Times of India linaripoti kwamba ushahidi ulioibiwa na tumbili huyo ni pamoja na kisu kinachoaminika kutumika katika mauaji hayo.

Polisi wa Jaipur wametuma barua kwa mahakama wakisema tumbili huyo alitoroka na ushahidi huo alipokuwa akielekea kwenye hifadhi.

Mahakama tayari imewataka polisi kuwasilisha ushahidi katika kesi ya mauaji ya Shashikant Sharma, ambaye alipatikana amefariki miaka sita iliyopita karibu na Kituo cha Polisi cha Chandwaji huko Jaipur.

Polisi walisema katika taarifa kwamba afisa huyo alikuwa amepumzika chini ya mti, kisha tumbili huyo akanyakua ushahidi huo na kutoweka.

Ghasia zilizuka baada ya siku kadhaa za mauaji ya Shashikant Sharma huko Jaipur, na polisi baadaye waliwakamata wanaume wawili, Rahul na Mohanlal Kandera, kutoka jiji hilo.

Mwendesha mashtaka pamoja na hakimu wa mahakama hiyo wanasemekana kughadhabishwa na uzembe wa polisi wa Jaipur, na wanasema hoja kwamba ushahidi kwamba uliibiwa na tumbili huyo si wa kawaida.

Haijulikani atafanya nini baada ya kuacha wadhifa huo.

Tukio lingine la kushtua lilitokea nchini India mwishoni mwa mwaka jana, baada ya maafisa kusema kuwa wamekamata nyani wawili kwa kuua karibu mbwa 250.

Shambulio hilo lilielezewa na Huduma ya Misitu ya India kama kulipiza kisasi kwa mauaji ya tumbili na mbwa