logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Njaa inasababisha kifo ’kila sekunde 48’ Katika Afrika Mashariki

Ripoti ya mashirika ya misaada yaashiria kuwa watu milioni 181 kote duniani wanakabiliwa na njaa

image
na Radio Jambo

Yanayojiri18 May 2022 - 05:54

Muhtasari


• Ripoti ya mashirika ya misaada Oxfam na Save the Children inakadiria kuwa takriban watu milioni 181 kote duniani wanapitia uzoefu viwango vya mzozo wa njaa.

 

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameonya juu ya njaa kali inayosababisha utapiamlo inayohusiana na mzozo, mzozo wa hali ya hewa, na mfumuko wa bei za chakula.

Mashirika ya kutetea haki za binadamu yameonya katika eneo lote la mataifa ya Ethiopia, Kenya na Somalia, mtu mmoja hufariki kila sekunde 48 kutokana na njaa ya muda mrefu inayosababishwa na mzozo, mzozo wa hali ya hewa na kuongezeka kwa gharama ya chakula.

Ripoti ya mashirika ya misaada Oxfam na Save the Children inakadiria kuwa takriban watu milioni 181 kote duniani wanapitia uzoefu viwango vya mzozo wa njaa, huku wanawake wakiathiriwa zaidi.

Mashirika hayo yanasema njaa kali ni kushindwa kisiasa.

Yanakosoa jamii ya kimataifa kwa kuchelewa sana kushugulikia tatizo la njaa na kutozuia dharura "zinazojirudia na kutabirika " .


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved