logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu wasiojulikana 'waiba makaburi' Msumbiji

Wahalifu hao wanaiba misalaba ya shaba na vitu vingine vya chuma

image
na Radio Jambo

Yanayojiri03 June 2022 - 09:42

Wakaazi wa mji wa Beira katika jimbo la kati la Msumbiji la Sofala wametaka ulinzi wa makaburi ya eneo hilo huku kukiwa na ripoti za uharibifu wa makaburi. Katika makaburi ya Mangalane, zaidi ya makaburi 50 yameharibiwa katika muda wa mwezi mmoja uliopita.

Wahalifu hao wanaiba misalaba ya shaba na vitu vingine vya chuma. Kiongozi wa kimila anayehusika na makaburi hayo, Fernando Jaime, alisema vitendo vya unajisi vimekuwa vikifanyika mchana kweupe.

"Wanachukua misalaba na vitu vingine vya watu waliokufa wanavyovikuta kando ya kaburi. Wanaweka vitu hivi pamoja na kuviuza kwa chakavu," aliambia vyombo vya habari vya ndani.

Carlos Cassicussa mkazi wa kitongoji cha Mungassa alisema hali hiyo inatokana na kuporomoka kwa maadili. “Hii tabia ni mbayakwa kweli, wizara ya mambo ya ndani ichukue hatua waje makaburini hata saa sita mchana,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved