logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waziri Mkuu wa zamani wa Japan Shinzo Abe amefariki-vyombo vya habari vya Japan

Abe, 67, ambaye anasalia kuwa waziri mkuu aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi nchini Japan,

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 July 2022 - 09:17

Muhtasari


  • Abe, 67, ambaye anasalia kuwa waziri mkuu aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi nchini Japan, alipigwa risasi alipokuwa akitoa hotuba ya kampeni

Waziri Mkuu wa zamani wa Japan Shinzo Abe amefariki, kwa mujibu wa shirika la habari la  kitaifa la Japan.

Abe, 67, ambaye anasalia kuwa waziri mkuu aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi nchini Japan, alipigwa risasi alipokuwa akitoa hotuba ya kampeni.

Mshambulizi anayeshukiwa - aliripotiwa kuwa mwanamume mwenye umri wa miaka 40 - alikabiliwa katika eneo la  tukio na kukamatwa.

Bw Abe alipigwa risasi mara mbili alipokuwa akitoa hotuba katika mji wa kusini wa Nara siku ya Ijumaa asubuhi.

Mara moja alianguka na kukimbizwa katika hospitali ya karibu. Picha zilizopigwa eneo la tukio zilimuonyesha akivuja damu. Maafisa wa usalama katika eneo la tukio walimkabili mshambuliaji huyo, na mshukiwa mwenye umri wa miaka 41 sasa yuko chini ya ulinzi wa polisi.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved